![]() |
Kambi ya Nyarugusu |
Kulingana na tume ya wakimbizi katika shirika la umoja wa Mataifa UNHCR wengi wa wakimbizi waliotorokea katika mataifa jirani wamelalamikia unyanyasaji ,wa kingono kukamatwa mara kwa mara,vitisho,kuajiriwa kujiunga na jeshi na mauaji.
Tanzania ina idadi kubwa ya wakimbizi wakiwemo raia 30 wa Burundi wanaoingia nchini humo kila siku na kambi ya Nyarugusu ni miongoni mwa kambi kubwa duniani ikiwa na wakimbizi 140,540.
Tume hiyo imesema kuwa idadi nyengine ya wakimbizi katika mataifa mengine ni kama ifuatavyo:
Rwanda (76,404)
DRC (22,204)
Uganda (24,583).
0 comments:
Post a Comment