Msichana wa tatu alikataa kushiriki katika shambulio hilo la Boko Haram na hii ni habari yake.
Huawa sio jina lake,hajui umri wake lakini anaonekana kuwa na kati ya miaka 17 na 18.
Alikamatwa na kundi la Boko haram kwa zaidi ya mwaka mmoja wakati watekaji wake walipopanga kushambulia kambi ya Dikwa.
![]() |
Bomu la mlipuaji wa kujitolea muhanga |
Badala yake ningependa kwenda kuishi na familia yangu hata iwapo nitakufa nikiwa huko,aliniambia kupitia mkalimani.
Wazazi wake wote na nduguze,isipokuwa kakaake moja ambaye alikuwa ametekwa pamoja naye walikuwa wakiishi katika kambi ya Dikwa katika jimbo la Borno,pamoja na wengine 50,000 waliotekwa kwa lazima katika makaazi yao.
Hauwa anaelezea vile alivyoshawishiwa kujiunga na kundi hilo.
Hatujui kile Hauwa alichokuwa akiugua,lakini mapepo hayo yalimfanya ajimwagie mchanga na hata kujichoma mkono wake.
Hivyobasi aliona Kundi la Boko haram kama jibu la matatizo yake na hivyobasi wakamchukua.
Anakumbuka siku moja akiishi na wapiganaji hao.
Baada ya mda fulani,Hauwa aliwachana na mumewe na akaolewa tena.
Mumewe wa pili alitoroka na alipokataa kuolewa na mume wa tatu kundi hilo lilipendekeza mpango wake.
''Walisema kwamba kwa sababu nimekataa kuolewa tena,nijilipue na bomu'',alisema.
Kambi hiyo ya Dikwa ya wakimbizi wa ndani kwa ndani ilikuwa kilomita 85 kaskazini mashariki mwa mji wa Maiduguri,mji mkuu wa jimbo la Borno na chimbuko la kundi la Boko Haram.
Hauwa aliijua kambi hiyo na alijua pia kwamba sio mbali na eneo analozuiliwa na wapiganaji hao,kwa hivyo usiku kabla ya shambulio hilo kufanyika alitoroka mapema asubuhi.
Alipokuwa karibu kufika katika kambi ya Dikwa wapiganaji wawili wa kujitolea muhanga walijilipua.
Afisa mmoja wa jeshi aliionyesha timu ya BBC eneo la shambulio hilo.
Mwanamke mmoja Falmata Mohammed anakumbuka dakika chache kabla ya shambulio.
Mwanajeshi mmoja alikuwa akijaribu kupanga foleni,na kulikuwa na mwanamke mmoja ambaye alikuwa amevalia kilemba chekundu na alikuwa na nywele ndefu.
mshirikishe mwenzako
0 comments:
Post a Comment