Serikali ya Sudan
Kusini imesema kuwa kiongozi wa waasi Riek Machar, amefutilia mbali
mpango wake wa kurejea Juba kwa muda usiojulikana.
Msemaji wa
serikali Michael Makuei amesema kuwa makamu wa bwana Machar, alitaka
kurejea Juba na silaha nzito nzito, zikiwemo, magari ya kivita,
makombora na bunduki nzito nzito.Aidha amesema kuwa serikali ya nchi hiyo tayari imeruhusu wanajeshi elfu moja mia tatu na sabini kati ya elfu moja mia nne na kumi kurejea Juba kuja kumlinda Bwana Machar.
Amesema kuwa utawala wa nchi hiyo hautaruhsu wanajeshi zaidi kurejeshwa Juba, kutokana na sababu za kiusalama
0 comments:
Post a Comment