Saturday, April 16, 2016

Mkuu wa shirika la UN amshutumu Trump


Trump mwishoni mwa mwaka jana alipendekeza Waislamu wazuiwe kuingia Marekani


Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Haki za Kibinadamu ameshutumu sera za mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani, akisema ni sawa na ushenzi.
Zeid Raad al-Hussein, ingawa hakumtaja Bw Trump moja kwa moja, alizungumzia hatua ya mfanyabiashara huyo tajiri kutoka New York kuunga mkono mateso pamoja na sera zake kali dhidi ya Waislamu.
“Ushenzi na ulokole si thibitisho la uongozi thabiti,” Hussein alisema.
Kamishna huyo pia amekosoa mpango wa mgombea mwengine Ted Cruz wa kuweka mpango wa kupeleleza maeneo wanamoishi Waislamu.
“Kutoa matamshi ya chuki, kuchochea na kuwatenga wengine si jambo la kuburudisha watu nalo, au jambo la kujifaidi kisiasa,” Bw Hussein ameambia hadhira katika mji wa Cleveland, Ohio.

Trump akemewa kwa matamshi kuhusu Waislam

 

 
Trump anaongoza kwenye kura za maoni miongoni mwa wagombea wa Republican
Vigogo wa chama cha Republican nchini Marekani wamemkemea mwenzao Donald Trump, anayetaka kuwania urais kupitia chama hicho, kwa kupendekeza Waislamu wazuiwe kuingia Marekani.
Mmoja wa wanaoshindani tiketi ya kuwania urais Jeb Bush amesema Bw Trump "mwenye kasoro akilini”. Makamu wa rais wa zamani Dick Cheney naye alisema pendekezo hilo "linaenda kinyume na yote ambayo huwa tunatetea”.
Ikulu ya White House, Umoja wa Mataifa na viongozi wa Kiislamu pia wamekosoa matamshi hayo ya Trump.
Bw Trump alikuwa amesema Waislamu wengi wana "chuki” dhidi ya Marekani.
Kwenye hotuba wakati wa kampeni, aliomba "Waislamu wote wazuiwe kuingia Marekani hadi wawakilishi wa nchi wajue ni nini kinachoendelea”
Meneja wake wa kampeni alisema marfuku hiyo ingeathiri "kila mmoja” bila kubagua kama ni mhamiaji au mtalii.


Lakini Bw Trump aliambia Fox News kwamba haingeathiri “watu wanaoishi humu nchini (Marekani), akiongeza kuwa Waislamu wanaohudumu katika jeshi la Marekani wangekaribishwa "nyumbani”.
Matamshi hayo ya Bw Trump yalitolewa Marekani ikiendelea kuomboleza kufuatia shambulio mbaya zaidi la kigaidi kutekelezwa tangu shambulio la Septemba 11, 2001.
Wiki iliyopita, wanandoa wawili Waislamu, ambao wanaaminika kukumbatia itikadi kali, walifyatua risasi na kuwaua watu 14 na kuwajeruhi wengine 21 katika kituo cha afya San Bernardino, jimbo la California.
Bw Trump alishangiliwa sana aliporudia ahadi yake katika mkutano wa kampeni jimbo la South Carolina saa chache baada ya kutoa matamshi hayo mara ya kwanza.

Ameongeza: "Mmoja wa wagombea wanaoongoza katika kinyang’anyiro cha kutaka kuwa rais wa nchi hii alitangaza, miezi kadha iliyopita, kujitolea kwake kutumia mateso (…) kuumiza watu wengine, ili watoe habari au wabuni habari ambazo hawazo nazo.”
Bw Hussein amesema si vyema kukiuka haki za wengine kujifaa kisiasa
Wakati wa kampeni, bw Trump alisema kwamba mateso wakati mwingine hufanikiwa na akaahidi kurejesha njia hatari zaidi kuliko kutumia maji kulazimisha washukiwa kufichua habari.
Njia hizo zilitumiwa na jeshi la Marekani katika washukiwa wa ugaidi lakini zilipigwa marufuku na utawala wa Bw Obama.



0 comments: