Friday, April 29, 2016

Wenger:Arsenal ilipoteza taji la ligi nyumbani

Arsene Wenger
Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger amesema kuwa timu yake ilipoteza harakati za kushinda ligi wakati wa kucheza mechi za nyumbani dhidi ya timu zilizo chini ye jedwali.
Arsenal iliopo katika nafasi ya nne imeshinda mechi sita kati ya mechi 16 ilizocheza.
Baadhi ya mashabiki wamemtaka raia huyo wa Ufaransa kuondoka katika mechi za hivi karibuni.
Ni lazima tujue kwamba ugenini tumekuwa washindi .
 Arsenal
Lakini nyumbani dhidi ya timu ndogo tulipoteza pointi nyingi,alisema Wenger.
Maandamano zaidi yanatarajiwa wakati wa mechi ya Jumamosi katika uwanja wa Emirates dhidi ya Norwich.

Trump achekwa kwa alivyotamka Tanzania

By on 12:47:00 PM
Trump alishambulia sana sera ya kigeni ya Obama


Mgombea urais wa chama cha Republican Donald Trump amekejeliwa mtandaoni baada ya kuonekana akiboronga akitamka Tanzania wakati wa kutoa hotuba.
Bw Trump alikuwa akizungumzia mashambulio ya kigaidi yaliyotekelezwa katika mabalozi ya Marekani nchini Kenya na Tanzania mwaka 1998 wakati wa kuzungumzia sera yake ya kigeni.
Badala ya kutamka vyema ‘Tanzania’ anasikika akitamka ‘Tan-zay-nia’.
Mashambulio hayo yalitekelezwa na mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda.
Msemaji wa ikulu ya White House pia alimcheka Bw Trump alipoulizwa kuhusu vile mfanyabiashara huyo tajiri kutoka New York alivyotamka jina Tanzania.
“Kweli, yamkini jinsi ya kutamka huwa haijaelezwa kwenye kifaa cha kuonesha maandishi ya hotuba,” alieleza afisa wa habari wa ikulu Bw Josh Earnest.

Magufuli: Polisi sharti wajirekebishe

By on 12:42:00 PM
Rais Magufuli amesema baadhi ya mambo yanachangia kuwepo kwa hali ngumu ya utendaji kazi Rais wa wa Tanzania Dkt John Magufuli amelitaka jeshi la polisi nchini pamoja na ofisi ya mwendesha mashitaka kujirekebisha katika utenda kazi na kujiepusha na kashfa.Amesema taarifa zinaonesha jeshi la polisi limekuwa likihusishwa na matumizi mabaya ya fedha hali inayoongeza ukubwa wa matatizo yanayokwamisha utendaji wake wa kazi.Akiongea alipokuwa akifungua kikao cha kazi cha makamanda wa polisi wa mikoa, mawakili wafawidhi wa serikali wa mikoa na wakuu wa upelelezi wa Mikoa na Vikosi, Dodoma ametoa mfano wa taarifa za matumizi mabaya ya fedha zinazotolewa kwa ajili ya kununulia vifaa na sare za askari.Aidha, amezungumzia mikataba yenye mashaka inayotiwa saini kati ya polisi na wawekezaji akisema baadhi ya mambo yanayoongeza hali ngumu ya utendaji kazi kwa jeshi hilo.“Nimesema lazima nizungumze kwa uwazi, nisiposema kwa uwazi nitajisikia vibaya nikimaliza mkutano huu, nataka muelewe na muelewe ukweli direction (njia) ninayoitaka mimi.”Dkt. Magufuli pia amelitaka jeshi la polisi kujiepusha na kashfa ambazo zimekuwa zikisemwa dhidi yake, ikiwemo maafisa wa polisi kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya na kuazimisha silaha kwa wahalifu wa ujambazi.Kuhusu Ofisi ya Mwendesha Mashitaka, amesema amekuwa akisikitishwa sana na vitendo vya serikali kushindwa katika kesi nyingi mahakamani licha ya kuwa na wanasheria mahiri."Niwaombe mawakili na polisi wanaohusika na upelelezi mtangulize maslahi ya nchi mbele, kwa sababu kumekuwa na usemi kwa baadhi ya wapelelezi na mawakili wachache, nasema wachache, panapokuwa na kesi inayohusiana na pesa pesa, wana misemo yao wanasema dili limepatikana,” amesema.“Na saa nyingine kesi inapopelekwa mahakamani wana-collude (wanakula njama) mawakili wa serikali na mawakili wanaomtetea mhalifu, na wanapo-collude (wanapokula njama pamoja) siku zote serikali inashindwa.”

Wednesday, April 27, 2016

Monday, April 25, 2016

Rwanda yawaondosha raia wake Zambia

Rwanda yawaondosha raia wake Zambia
Raia 13 wa Rwanda wamekuwa wa kwanza kurejeshwa Kigali kufuatia kutibuka kwa ghasia dhidi yao nchini Zambia.
Serikali ya Rwanda imechukua hatua hiyo kufuatia ghasia zilizowalenga wanyarwanda na biashara zao nchini Zambia.
Waliorejea nchini Rwanda ni watu 13 walioweza kufika kwenye afisi za ubalozi wa Rwanda mjini Lusaka na ambao mali zao iliteketezwa kabisa.
Katika mazungumzo na BBC wanyarwanda hao wanasema mali zao nchini Zambia ziliteketezwa na kwamba hali ya maisha nchini Rwanda itakuwa ngumu kwa kuwa walikuwa wameishauza mali zao kabla ya kuwekeza nchini Zambia.
Mmoja wa wanyarwanda hao Alfani Sindaheba amesema kuna uhasama na chuki dhidi ya wageni Zambia.
Ameongeza kuwa sababu nyingine inaweza kuwa ya kisiasa hasa mbinu za wapinzani kutaka kumharibia sifa rais Edgar Lungu.

 Polisi walikuwa na wakati mgumu kudumisha hali ya amani


“mwezi wa 8 kutafanyika uchaguzi na huyu rais baadhi hawampendi kwa sababu alipofika madarakani alibadilisha mambo mengi na dolla ya Marekani ikapanda sana,hivyo wengi hawakupendezwa na mageuzi aliyoyafanya.'
''Nafikiri baadhi ya wanasiasa wametumia machafuko haya ya chuki dhidi ya wageni kutaka kumvuruga rais Lungu.”alisema Bwana Sindaheba.
Wanyarwanda hao waliorejea kutoka Zambia baadhi wamesafirishwa katika maeneo yao asilia na wengine wamesalia hotelini mjini Kigali,wakisubiri mipango ya serikali ya kuwasafirisha hadi mikoa yao asilia.

Tuesday, April 19, 2016

Salamu TMK - Mfuko Official Video





karibu upate uhondo


                                                        downlod hapa

Atolewa kwenye ndege kwa kuongea Kiarabu

By on 12:54:00 PM
Mwanafunzi wa chuo kikuu raia wa Iraq katika jimbo la California nchini Marekani anasema kuwa alitolewa kutoka kwenye ndege ya shirika la ndege la Southwest baada ya kufanya mazungumzo kwa lugha ya kiarabu.
Shirika hilo la Southwest lilisema kuwa Khairuldeen Makhzoomi aliondolewa ndegeni tarehe 9 mwezi Aprili kabla ya ndege hiyo kupaa.
Bw Makhzoomi anasema alikuwa akizungumza na mjomba wake kwa njia ya simu kuhusu hotuba ya katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon.
Anasema kuwa mwanamke mmoja kwenye ndege hiyo alimkodolea macho wakati alitamka jina "Inshallah" akimaanisha Mungu akipenda.
Baada ya kutumia jina hili mfanyikazi wa shirika la Southwest alimsindikiza nje ya ndege.
Bw Makhzoomi ambaye aliingia nchini Marekani kama mkimbizi kutoka Iraq na sasa ni mwanafunzi wa chuo cha Carlifonia cha Berkeley, aliambiwa kuwa hawezi kuingia tena kwenye ndege hiyo.
By on 12:47:00 PM
Raia waliolazimika kutoka nje ya mahakama baada ya ombi la kuisikiza kesi hiyo kwa faragha kukubaliwa
Mahakama mjini Kigali imeanza kusikiliza kesi ya rufaa iliyowasilishwa na kundi la waislamu wakipinga kifungo cha muda katika kesi inayohusu ugaidi.
Kundi hilo linatuhumiwa makosa ya kuhamasisha na kusajili wapiganaji wa kujiunga na kundi la IS nchini Syria.
Watuhumiwa 11 miongoni mwa 17 ndio wamejitokeza mahakamani.
Kinyume na ilivyokuwa awali usalama haukuwa mkali kiasi kwamba watuhumiwa waliweza kuongea na jamaa zao waliokuwepo kuwaunga mkono.
Washtakiwa na mawakili wao walitaka mahakama kupinga uamuzi uliochukuliwa na mahakama ya mwanzo wa kuwapa kifungo cha muda cha siku 30 badala yake wakataka kesi yao isikilizwe wakiwa nje ya kizuizi.
Hakuna mengi yaliyosikilizwa kwani kabla ya hoja za kesi hiyo kuendelea,mwendesha mashitaka ameomba mahakamani kesi hiyo isikilizwe kwa faragha.
Jaji ameunga mkono ombi hilo na kuwataka waliohudhuria kesi kutoka nje isipokuwa washitakiwa na mawakili wao.
Katika kesi ya awali,watuhumiwa walikana mahusiano ya aina yoyote na kundi la Islamic State na kwamba kamwe hawajashiriki mafunzo yoyote ya kijeshi kwa lengo la kusaidia kundi hilo kama yalivyo mashitaka dhidi yao.
Mahakama ya mwanzo ilikuwa imechukua uamuzi wa kuwaweka kizuizini kwa muda ikizingatia ushahidi wa marehemu Imam Mohamed Mugemangango aliyeuawa mwezi wa kwanza mjini Kigali kwa kupigwa risasi na polisi kwa madai kuwa alitaka kutoroka.
Imetangazwa kwamba katika ngazi Imamu huyo alikuwa ametangaza kuwa watuhumiwa hao ni kundi linalotafuta vijana wa kujiunga kundi na Islamic State na wako tayari kufanya Jihad.
Lakini wao wanasema ushahidi wa mtu aliyekufa hauwezi kuzingatiwa.
Kesi itaendelea kusikilizwa kwa faragha

Machar afuta mpango wa kurejea Juba

By on 12:43:00 PM
https://www.blogger.com/blogger.g?blogID=6465176323126612680#editor/target=post;postID=925816011096298285


Serikali ya Sudan Kusini imesema kuwa kiongozi wa waasi Riek Machar, amefutilia mbali mpango wake wa kurejea Juba kwa muda usiojulikana.
Msemaji wa serikali Michael Makuei amesema kuwa makamu wa bwana Machar, alitaka kurejea Juba na silaha nzito nzito, zikiwemo, magari ya kivita, makombora na bunduki nzito nzito.
Aidha amesema kuwa serikali ya nchi hiyo tayari imeruhusu wanajeshi elfu moja mia tatu na sabini kati ya elfu moja mia nne na kumi kurejea Juba kuja kumlinda Bwana Machar.
Amesema kuwa utawala wa nchi hiyo hautaruhsu wanajeshi zaidi kurejeshwa Juba, kutokana na sababu za kiusalama

Monday, April 18, 2016

Filamu nyingine ya Avatar kuongezwa

Filamu ya kwanza ya Avatar ilitolewa 2009 na iliwashirikisha Sam Worthington na Zoe Saldana

Watengenezaji wa filamu ya Avatar franchise wamesema kutatolewa filamu zaidi katika mwendelezo huo wa filamu, filamu ijayo ikitarajiwa kutolewa 2018.
Mwelekezi wa filamu hizo James Cameron ametangaza kwamba filamu hizo zitaendelezwa hadi makala ya tano itakayotolewa 2023.
Alikuwa tayari amethibitisha kwamba filamu tatu zaidi zingetolewa lakini amefichua kwamba kuna mambo mengi sana ya kuelezwa kwenye hadithi hiyo na makala zijazo tatu hazitoshi.

Kote duniani, Avatar inasalia kuwa filamu iliyofanikiwa zaidi katika historia.Filamu hiyo imezoa $2.7bn tangu kutolewa wake 2009.Filamu ijayo ya Avatar itatoka 2018, na hizo nyingine 2020, 2022 na 2023.

Boko Haram wavamia kambi ya jeshi Nigeria



Wapiganaji wa kundi la Boko Haram wameishambulia kambi ya jeshi la Nigeria mapema asubuhi ya leo na kuua idadi kubwa ya wanajeshi huko Borno.

 .Mwanajeshi mmoja aliyeko Borno ameielezea BBC kuwa''wapiganaji wa Boko Haram waliwavizia na kuwashambulia alfajiri na mapema wakiwa wamelala.''''Wapiganaji hao walikuwa wamejihami kwa silaha kali na kusababisha maafa makubwa upande wa wanajeshi''
''Tuliwapoteza wenzetu wengi,,,,,wengi sana,, sijui hata ni wangapi waliojeruhiwa'' alisema mwanajeshi huyo ambaye hakutaka kutajwa jina lake
Kambi hiyo ndogo iliyoko katika kijiji cha Kareto ilikuwa na wanajeshi wachache ambao kazi yao ilikuwa ni kulinda ngome kabla ya kikosi kikubwa zaidi kuwasili.
Hata hivyo mwanajeshi huyo anasema kuwa idadi ya wapiganaji hao ilikuwa kubwa mno hata wanajeshi kadhaa walitoroka ilikuokoa maisha yao.
''Walikuwa na silaha nzito nzito na kali kuliko zetu'' afisa huyo aliiambia idhaa ya BBC Hausa.
 
Mwanajeshi mmoja aliyeko Borno ameielezea BBC kuwa''wapiganaji wa Boko Haram waliwavizia na kuwashambulia alfajiri na mapema wakiwa wamelala.''
''Tuliwapoteza wenzetu wengi,,,,,wengi sana,, sijui hata ni wangapi waliojeruhiwa''
''Baadhi yetu walitoroka maji yalipozidi unga''
''Tuligundua idadi ya wavamizi ilikuwa ni kubwa kuliko yetu'' mwanajeshi mwengine aliiambia shirika la habari la AFP.
 
''Walikuwa na silaha nzito nzito na kali kuliko zetu'' afisa huyo aliiambia idhaa ya BBC Hausa.
Wapiganaji kadhaa waliuawa katika makabiliano hayo yaliyodumu kwa saa kadhaa kulingana na wenyeji wa kijiji hicho.
Hata hivyo jeshi lilijitahidi na kuikomboa kambi hiyo baada ya mashambulizi ya angani kuwasili na kuwaokoa wanajeshi walikuwa wamesakamwa ardhini.
Idadi kamili ya waliouawa haijajulikana.

Korea Kaskazini kulipua bomu la nyuklia

By on 10:09:00 AM
Korea Kaskazini ilifanyia majaribio bomu la haidrojeni Januari mwaka huu

Korea Kusini imesema imepata dalili kwamba Korea Kaskazini inajiandaa kufanya jaribio la tano la bomu la nyuklia, Rais Park Geun-hye amesema.
Hakufafanua zaidi kuhusu dalili hizo, lakini ameagiza jeshi la nchi yake kuwa tayari, shirika la habari la nchi hiyo limesema.
Kumekuwa na ripoti katika vyombo vya habari nchini Korea Kusini kwamba kumeongezeka shughuli katika kituo cha majaribio ya silaha za nyuklia cha Korea Kaskazini cha Punggye-ri, ambapo majaribio ya awali yalitekelezwa.
Iwapo Pyongyang itaendelea na kufanyia majaribio bomu la nyuklia, basi itakuwa ni kukaidi zaidi vikwazo vikali ilivyoongezewa na Umoja wa Mataifa mwezi jana.
"Tupo katika hali ya kutatanisha, hatujui iwapo Korea Kaskazini inaweza kufanya uchokozi kama njia ya kujitetea kutokana na kutengwa na jamii ya kimataifa na pia kuimarisha uungwaji mkono ndani ya nchi,” Bi Park aliambia maafisa wake wakuu wa jeshi, shirika la habari la Yonhap liliripoti
Mwezi Januari, Korea Kaskazini ilifanya jaribio la nne la silaha za nyuklia na baadaye ikarusha kombora baharini.
 
Kituo cha Punggye-ri
 
Hatua hiyo iliongeza hali ya wasiwasi katika rasi ya Korea.Waangalizi wanasema huenda jaribio hilo la bomu likafanywa kabla ya mkutano mkuu wa chama tawala cha Workers' Party mjini Pyongyang mwezi Mei.
Wataalamu wanaamini Korea Kaskazini haina uwezo wa kiteknolojia wa kuweka silaha ya nyuklia kwenye kombora, ingawa imepiga hatua kubwa katika mpango wake wa nyuklia miaka ya karibuni.

UN: Burundi inawatesa wapinzani wake

By on 10:03:00 AM
Idadi ya watu wanaoteswa nchini Burundi imeongezeka maradufu.


Idadi ya watu wanaoteswa nchini Burundi imeongezeka maradufu.
Umoja wa mataifa unasema kuwa katika kipindi cha miezi mitatu ya kwanza mwaka huu takriban watu 400 wameripotiwa kukamatwa na vyombo vya dola na kisha kuteswa..
Zeid Ra'ad Al Hussein anasema kuwa mawakala wake wamerekodi visa 345 za mateso na dhulma dhidi ya watu wanaokisiwa kuwa wapinzani nchini Burundi.

 
Mkuu wa kitengo cha haki za binadamu wa Umoja huo wa Mataifa Zeid Ra'ad Al Hussein anasema kuwa mawakala wake wamerekodi visa 345 za mateso na dhulma dhidi ya watu wanaokisiwa kuwa wapinzani nchini Burundi.
Tangu machafuko ya kisiasa yalipoanza mwaka mmoja uliopita, takriban watu 600 wameshikwqa na kuteswa na vyombo vya serikali ya rais Pierre Nkurunziza.
 
Add caMachafuko yalianza nchini Burundi rais Pierre Nkurunziza alipotangaza nia yake ya kuwania muhula wake wa tatu . ption
''Hao ndio waliokuwa na shime ya kujitokeza ,tunashuku kuwa idadi ya wale walioteswa ni kubwa mno ila kutokana na hofu ya kukabiliwa na maafisa wa usalama wengi wanajificha'' alisema afisa huyo wa UN.
Wale wanaokamatwa na kuteswa mara nyingi wanasema kuwa wanapitia dhulma hiyo ndani ya vituo vya idara ya usalama wa taifa na kijasusi ya Burundi.
Hadi kufikia sasa takriban watu 400 wamethibitishwa kufariki

 
Machafuko yalianza nchini Burundi rais Pierre Nkurunziza alipotangaza nia yake ya kuwania muhula wake wa tatu .
Rais Pierre Nkurunziza
 
 
Wapinzani wake walimkashifu kwa kukiuka katiba ya taifa huku rais mwenyewe akisisitiza kuwa wala hakukiuka kamwe katiba kwani muhula wa kwanza , alipoongoza taifa hilo hakuchaguliwa na umma bali wajumbe wa kamati maalum ya upatanisho iliyoundwa kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe 2005.
Hadi kufikia sasa takriban watu 400 wamethibitishwa kufariki huku zaidi ya watu laki mbili u nusu wakilazimika kutorokea mataifa jirani kwa hofu ya kuzuka mapigano mapya.

Saturday, April 16, 2016

Mkuu wa shirika la UN amshutumu Trump


Trump mwishoni mwa mwaka jana alipendekeza Waislamu wazuiwe kuingia Marekani


Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Haki za Kibinadamu ameshutumu sera za mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani, akisema ni sawa na ushenzi.
Zeid Raad al-Hussein, ingawa hakumtaja Bw Trump moja kwa moja, alizungumzia hatua ya mfanyabiashara huyo tajiri kutoka New York kuunga mkono mateso pamoja na sera zake kali dhidi ya Waislamu.
“Ushenzi na ulokole si thibitisho la uongozi thabiti,” Hussein alisema.
Kamishna huyo pia amekosoa mpango wa mgombea mwengine Ted Cruz wa kuweka mpango wa kupeleleza maeneo wanamoishi Waislamu.
“Kutoa matamshi ya chuki, kuchochea na kuwatenga wengine si jambo la kuburudisha watu nalo, au jambo la kujifaidi kisiasa,” Bw Hussein ameambia hadhira katika mji wa Cleveland, Ohio.

Trump akemewa kwa matamshi kuhusu Waislam

 

 
Trump anaongoza kwenye kura za maoni miongoni mwa wagombea wa Republican
Vigogo wa chama cha Republican nchini Marekani wamemkemea mwenzao Donald Trump, anayetaka kuwania urais kupitia chama hicho, kwa kupendekeza Waislamu wazuiwe kuingia Marekani.
Mmoja wa wanaoshindani tiketi ya kuwania urais Jeb Bush amesema Bw Trump "mwenye kasoro akilini”. Makamu wa rais wa zamani Dick Cheney naye alisema pendekezo hilo "linaenda kinyume na yote ambayo huwa tunatetea”.
Ikulu ya White House, Umoja wa Mataifa na viongozi wa Kiislamu pia wamekosoa matamshi hayo ya Trump.
Bw Trump alikuwa amesema Waislamu wengi wana "chuki” dhidi ya Marekani.
Kwenye hotuba wakati wa kampeni, aliomba "Waislamu wote wazuiwe kuingia Marekani hadi wawakilishi wa nchi wajue ni nini kinachoendelea”
Meneja wake wa kampeni alisema marfuku hiyo ingeathiri "kila mmoja” bila kubagua kama ni mhamiaji au mtalii.


Lakini Bw Trump aliambia Fox News kwamba haingeathiri “watu wanaoishi humu nchini (Marekani), akiongeza kuwa Waislamu wanaohudumu katika jeshi la Marekani wangekaribishwa "nyumbani”.
Matamshi hayo ya Bw Trump yalitolewa Marekani ikiendelea kuomboleza kufuatia shambulio mbaya zaidi la kigaidi kutekelezwa tangu shambulio la Septemba 11, 2001.
Wiki iliyopita, wanandoa wawili Waislamu, ambao wanaaminika kukumbatia itikadi kali, walifyatua risasi na kuwaua watu 14 na kuwajeruhi wengine 21 katika kituo cha afya San Bernardino, jimbo la California.
Bw Trump alishangiliwa sana aliporudia ahadi yake katika mkutano wa kampeni jimbo la South Carolina saa chache baada ya kutoa matamshi hayo mara ya kwanza.

Ameongeza: "Mmoja wa wagombea wanaoongoza katika kinyang’anyiro cha kutaka kuwa rais wa nchi hii alitangaza, miezi kadha iliyopita, kujitolea kwake kutumia mateso (…) kuumiza watu wengine, ili watoe habari au wabuni habari ambazo hawazo nazo.”
Bw Hussein amesema si vyema kukiuka haki za wengine kujifaa kisiasa
Wakati wa kampeni, bw Trump alisema kwamba mateso wakati mwingine hufanikiwa na akaahidi kurejesha njia hatari zaidi kuliko kutumia maji kulazimisha washukiwa kufichua habari.
Njia hizo zilitumiwa na jeshi la Marekani katika washukiwa wa ugaidi lakini zilipigwa marufuku na utawala wa Bw Obama.



Tetemeko la pili laikumba Kumamoto, Japan

By on 12:49:00 AM
Tetemeko hilo lilisababisha kuporomoka kwa majengo

Maafisa nchini Japan wanasema kuwa tetemeko kubwa la ardhi limewaua takriban watu 19 na kusababisha uharibifu mkubwa.
Tatemeko hilo ambalo ni la pili kukumba kisiwa cha Kyushu ndani ya siku mbili, limesababisha kuporomoka kwa majengo, limeharibu barabara pamoja na mifumo ya maji na umeme.
Tetemeko hilo lilikuwa na nguvu ya 7.3 kwenye vipimo vya Richter.
Tetemeko hilo la ardhi, ambalo chanzo chake ni kilomita 10 chini ya ardhi karibu na mji wa Kumamoto, lilikuwa kubwa na liliathiri eneo kubwa kuliko la kwanza lililotokea katika mji huo wa Kumamoto Alhamisi usiku.
Watu wengi wamejeruhiwa
Afisa wa serikali wa Kumamoto Tomoyuki Tanaka ameambia AP kwamba idadi ya waliofariki inatarajiwa kuongezeka.
Wanajeshi 20,000 wametumwa kusaidia juhudi za uokoaji lakini jitihada za uokoaji zimetatizwa na mitetemeko mingine midogomidogo.
Waziri mkuu Shinzo Abe amekuwa na mipango ya kuzuru ki