Friday, December 11, 2015

Thursday, December 3, 2015

Well come in talanta group olasity Kati arusha Tanzania we produce good instruments for water management like ports. Tank ect

                                                     tok

kwa maelezo piga sm 0759894855

Tuesday, December 1, 2015

Marekani kutuma jeshi kushambulia IS

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Ash Carter amesema jeshi maalum la Marekani litatumwa kwenda nchini Iraq kupambana na wapiganaji wa Islamic State katika nchi za Iraq na Syria.
Amesema majeshi hayo yatafanya operesheni hiyo ikiwa ni pamoja kuwaokoa mateka na kuwakamata viongozi wa I S.
Wakati huo huo Rais wa Syria Bashar Al Assad amesema uamuzi wa Urusi kuingia vitani katika nchi yake kumedhoofisha nguvu ya wapigani wa Islamic state tofauti na majeshi ya Marekani ambayo yamefanya kundi hilo kujiimarisha zaidi.
Waziri huyo wa ulinzi wa Marekani Ash Carter alitoa kauli hiyo wakati akiongea kwenye Kamati ya Congress huko Washtong nchini Marekani.
"Kuongeza kasi hiyo tutatuma tena kwa amri ya rais Obama na kwa ushauri wa mwenyekiti na wangu, Kikosi maalum cha kijeshi nchini Syria kusaidia kupambana na wapiganaji wa ISIL. Majeshi hayo maalum ya uwezo maalum wa kufanya kazi mbali mbali. Litatusaisia kufanya upelelezi wa ardhini kusaidia majeshi ya nchi hizo na watarudisha maeneo yaliyochutekwa na ISIL. Mahali tutakapopata nafasi kuteka maeneo tutapanua harakati zaidi."
Aidha Cater amesema katika maeneo ya Iraq majeshi hayo yatapambana na vilivyo na wapiganaji wa Islamic State.
"Kwa uratibu kamili na serikali ya Iraq tutapeleka majeshi maalum kupambana kwa kusaidia majeshi ya Iraq na wapiganaji wa Peshmega kuzidi kuwashughulikia ISIL. Majeshi haya maalum kwa muda wote watakuwa na uweza wa kuendesha opesheni kuwaachia huru mateka kukusanya taarifa za kiusalama na kuwakamata viongozi wa ISIL."
Wakati huo huo Rais wa Syria Bashar Al Assad amesema uamuzi wa Urusi kuingia vitani katika nchi yake imebadilisha hali katika uwanja wa vita. Katika mahojiano kwenye kituo cha televisheni cha Czech Assad amesema tangu Urusi ilipoingilia kati kijeshi wapigani wa Islamic State na makundi mengine ya jihad yamedhoofika, na amesema anaamini msaada wa Urusi utaendelea. Amesema majeshi ya Urusi yamekuwa na uwezo na uamuzi wa hali ya juu tofauti na majeshi ya ushirika yanayoongozwa na Marekani.
Katika hatua nyingine naye Waziri Mkuu wa Uingereza amewaomba wabunge wa chama cha Conservative kuunga mkono mpango wake wa majeshi ya Uingereza kufanya mashambulizi ya angani dhidi ya Islamic State nchini Syria.

Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na uongozi wa TRA na TPA alipofanya ziara ya kustukiza Bandarini leo asubuhi.



Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na uongozi wa TRA na TPA alipofanya ziara ya kustukiza Bandarini leo asubuhi.
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa leo ameamuru kukamatwa kwa maafisa kadhaa  wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na wengine kufukuzwa kazi  baada ya kufanya ziara ya kushtukiza Bandarini na kukuta madudu ambayo hakuyafurahia.
Maafisa hao, ambao kwa sasa tunahifadhi majina ili Jeshi la Polisi liweze kuwashughulikia, wametakiwa pia kusalimisha hati zao za usafiri.
Hii imekuja baada ya kugundulika kwamba kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.







               Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa TRA na TPA

Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa 
akiagana na viongozi wa TRA na TPA.

BAT 'iliwahonga' viongozi Afrika Mashariki

Uchunguzi wa shirika la habari la BBC umegundua kuwa kampuni ya kutengeneza sigara ya British American Tobacco (BAT) imekuwa ikitoa hongo kwa wakuu serikalini katika mataifa ya kanda ya Afrika Mashariki kwa nia ya kuwashawishi kubadilisha sheria ilikulinda biashara ya tumbaku licha ya madhara yake kwa afya ya wavutaji.
Ufichuzi huo umeibuka baada ya mfanyikazi mmoja kuipatia BBC stakabadhi zinazofichua ufisadi huo.
BAT ilipoulizwa kuhusu ukweli wa madai hayo ya ufisadi iliiambia BBC kuwa
''Ukweli ni kuwa hatushiriki ufisadi kwa namna yeyote katika mataifa yeyote tunayohudumu''
Paul Hopkins, ambaye aliifanyia kazi kampuni hiyo ya BAT, nchini Kenya kwa miaka 13 anasema kuwa alianza kutoa hongo baada ya kuambiwa kuwa hiyo ni gharama ya kufanya biashara barani Afrika
"ukweli ni kwamba ikiwabidi kuvunja sheria ilikufaulu katika biashara huwa wanavunja sheria''
barua pepe zilizotumwa na Hopkins zinaonesha vipi mawasiliano yalianza na jinsi malipo yalivyotolewa.
Aidha Hopkins anaonesha jinsi BAT ilivyowapa hongo maafisa wa shirika la afya duniani WHO ambao wanasimamia udhibiti wa matumizi ya tumbaku ilikupunguza idadi ya watu wanaopoteza maisha yao kutokana na maradhi yanayotokana na matumizi ya mmea huo.
BURUNDI
Afisa mmoja wa FCTC nchini Burundi, Godefroid Kamwenubusa,na mwakilishi wa visiwa vya Comoros , Chaibou Bedja Abdou, walilipwa kiinua mgongo cha dola $3,000 (£2,000).
Wakati huohuo mwakilishi wa Rwanda, Bonaventure Nzeyimana, akatia kibindoni dola elfu $20,000.




Wote hao wamekanusha kupokea hongo kutoka kwa BAT.
RWANDA
Dakta Vera Da Costa e Silva, wa WHO, ameilaumu BAT na kusema kuwa "ni jambo la kufedhehesha sana''.
"hii ni unyama, kutumia fedha ilikupata faida huku maisha ya watu yakiangamia'' BAT sharti iadhibiwe vikali na serikali alisema bibi huyo.
BAT kimsingi iliwatumia watu waliopokea hongo kubadilisha sheria za nchi husika ilikuzuia biashara hiyo ya tumbaku isiathirike.
Kwa mfano wakala wa kampuni hiyo anasema katika moja ya nyaraka za siri kuwa Bwana Kamwenubusa atafuatilia na kufanikisha mabadiliko muhimu kabla rais wa nchi hiyo kutia sahihi na kuifanya kuwa sheria.
Comoros
Nchini Uingereza ni hatia kutoa hongo hata kama matukio hayo ya rushwa yalifanywa katika mataifa mengine.
BAT kwa upande wake inajitetea kwa kusema kuwa wafanyikazi wake walifanya makosa kinyume na maadili ya kampuni hiyo.
"Tunawahakikishia kuwa tunachunguza madai haya kwa nia ya kuadhibu wale watakaopatikana na hatia ya kukiuka maadili ya BAT''
''Wale wanaotoa madai hayo ni wafanyikazi wetu waliotimuliwa na hivyo tunahisi hizi ni njama za kulipiza kisasi''
Bwana Hopkins anasikika katika ukanda ulionaswa kisiri akimshauri wakili wa kampuni hiyo kuwa watu kadhaa watahitajika kulipwa ilikufunga vivywa vyao.
Wakili huyo Naushad Ramoly, anasikika akiuliza iwapo kuna watu wengine wanaostahili kulipwa ?''
Ramoly ambaye sasa hafanyikazi na BAT anasema kuwa hakushiriki ukiukaji wa maadili yeyote na wala hakuhusika katika shughuli zozote zinazokiuka sheria na kanuni''




Aliyeua na kuchapisha kwa Facebook kufungwa

wanaume mmoja aliyeua mkewe na kuchapisha picha yake kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook amepatikana na hatia ya mauaji.
Derek Medina mwenyeji wa Florida Marekani alipatikana na hatia ya kumpiga risasi 8 Jennifer Alfonso nyumbani kwao baada ya majibizano makali.
Kiongozi wa mashtaka wa jimbo la Miami-Dade,Katherine Rundle amesema inaudhi kuwa mwanamme mkatili anaweza kumpiga risasi mwanamke na kisha kuchapisha picha kwenye mtandao wa kijamii.


Medina alidai kuwa mkewe mwenye umri wa miaka 27 alikuwa ametishia kumdunga kisu. 

 wanaume mmoja aliyeua mkewe na kuchapisha picha yake kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook amepatikana na hatia ya mauaji.
Derek Medina mwenyeji wa Florida Marekani alipatikana na hatia ya kumpiga risasi 8 Jennifer Alfonso nyumbani kwao baada ya majibizano makali.
Kiongozi wa mashtaka wa jimbo la Miami-Dade,Katherine Rundle amesema inaudhi kuwa mwanamme mkatili anaweza kumpiga risasi mwanamke na kisha kuchapisha picha kwenye mtandao wa kijamii.









Idadi ya vijana wanaokataa kwenda shule kwa sababu ya kujishughulisha na uchumaji upakiaji wa matawi yake

Idadi ya vijana wanaokataa kwenda shule kwa sababu ya kujishughulisha na uchumaji upakiaji wa matawi yake.

Hata hivyo utafiti katika maeneo yanayokuzwa mumea huu umetambua kuwa idadi ya vijana wanaokataa kwenda shule kwa sababu ya kujishughulisha na uchumaji wa Miraa na upakiaji wa matawi yake.
''kutokana na utashi wa bidhaa hiyo,malipo ya wafanyikazi wanaoishughulikia ni ya juu mno kwa hivyo inawavutia vijana kuacha masomo alisema daktari huyo.
Daktari Lukoye Atwoli alisema kuwa miraa husababisha walaji wake kuwa na mori na hata wakati mwengine msongo wa mawazo.
Utafiti huu unafwatia ule uliofanywa mwaka uliopita na wataalamu kutoka chuo kikuu cha Nairobi kwa ushirikiano na chuo kikuu cha Konstanz cha Germany na kile cha Minnesota, Marekani uliobaini kuwa ulaji wa miraa unaathiri ubongo wa walaji wake na kusababisha msongo wa mawazo,mafadhaiko na mahangaiko ya kiakili mbali na matatizo mengine chungu nzima.

 

Utafiti:Ulaji wa miraa unapunguza nguvu za kiume

Ulaji wa Miraa unaathiri nguvu za kiume.
Utafiti uliofanywa kwa niaba ya serikali ya Kenya na wahadhiri wa chuo kikuu cha Moi kilichoko katika Bonde la ufa umebaini kuwa Majani ya miraa inayofahamika pia kama 'Mairungi' unazuia ukuaji wa manii.
Aidha ulaji wa kipindi kirefu wa miraa unafanya mbegu za kiume za wanaume kufa haraka pindi zinapowekwa kwenye uke.
Mtafiti mkuu wa chuo kikuu cha Moi, Ochiba Lukanda, anasema kuwa utafiti sawa na huo uliofanywa huko ghuba ulibaini matokeo kama hayo.
Lukanda anasema kuwa wanaume ambao wamekuwa wakila Miraa kwa kipindi kirefu na wakaacha huwa wanapata uwezo wao wa kutunga mimba.
Ulaji wa Miraa pia huwa unasababisha mshtuko wa moyo.
''Mtu anapokula mmea huu baada ya muda damu yake huaanza kwenda kwa kasi, mbali na shinikizo la damu mumea huu hausababishi saratani kama inavyodaiwa '' Dakta Lukanda

Friday, November 20, 2015

Je,unataka kuvunja uhusiano wako kwa urahisi?


             Uhusiano katika facebook 

Hakuna hisia mbaya zaidi inayokujia wakati unapokutana na chapisho linalokuhusisha wewe na mpenzi wako wa zamani mukijifurahisha.
Ni vibaya zaidi unapogundua kwamba jina la pili la mpenzi huyo wa zamani limebadiliswa.
Hatahivyo kuna habari njema,mtandao wa facebook umetangaza kuwa unatafuta mbinu mpya ya kupunguza machungu unayopata wakati unapokutana na mpenzi wa zamani ambaye muliwachana baada ya ugomvi.
Kwa sasa,iwapo hutaki kukumbushwa kuhusu mpenzi huyo wa zamani una uwezo wa kumuondoa kama rafiki ama hata kumzuia asiweze kukuona katika mtandao wa facebook.

  •  kifaa kipya cha facebook
Tatizo ni kwamba watajua kwamba umechukua hatua kama hiyo ambayo sio nzuri sana.
Mahusiano katika mtandao wa facebook ni swala muhimu sana,kama alivyosema jaji mmoja kutoka mjini New York, kwamba unaweza kutuma wito wa talaka katika mtandao huo na uwe halali.
Lakini kifaa kipya cha mtandao wa facebook kinalenga kubadilisha kile ambacho mpenzi wako wa zamani anaweza kuona,bila kujua kwamba kuna kitu umefanya..
Kipengele hicho kinaruhusu:
*Kutoliona mara kwa mara jina la mpenzi wa zamani pamoja na picha yake bila kuiondoa ama kumzuia kukuona.
 Facebook


*Machapisho yao hayataonekana na majina yao hayatorodheshwa wakati watu wanapoandika ujumbe mpya ama hata kuwasambazia marafiki picha zao.
*Zuia picha ,video ama hata machapisho yoyote ambayo mpenzi wako wa zamani anaweza kuyaona.
*Weka usimamizi wa ni nani anayeweza kuona picha zako na mpezi wako wa zamani na uziondoe katika machapisho yenu pamoja.
*Wakati facebook ilipozinduliwa katika taasisi na vyuo vikuu,lengo lake lilikuwa machapisho ya mahusiano.Ni hatua ya kidijitali ambayo ilisaidia mda wa wengi.

                                                Kifaa kipya cha Fecbook
Lakini hivi majuzi,watu wamekuwa wakichukua tahadhari wanapotangaza uhusiano wao katika facebook.
Watu walikuwa wakitumia neno ''its complicated'' kwa uhusiano ambao unaelekea kugonga mwamba na badala yake watu wanatumia maneno ya kidunia kama vile 'kuchumbiwa' ama hata 'kupata mtoto'.
Hatahivyo kifaa hicho kipya kitaanza kutumika hivi karibuni,imesema facebook.


      Facebook

Mpango huo ni mongoni mwa juhudi zinazoendelea kuendeleza raslimali za watu wanaokabiliwa na wakati mgumu katika maisha yao,aliandika Kelly Winters meneja msimamizi wa bidhaa za facebook.
''Tunaamini kifaa hicho kitawasaidia watu kumaliza uhusiano wao katika facebook kwa urahisi na udhibiti.Iwapo unatumia simu ya mkononi nchini Marekani unaweza kukitumia kifaa hicho mara moja kwa kuvunja uhusiano na mpenzi wako''.

Facebook yaonywa ikome kudukua Ubelgiji

Mahakama moja nchini Ubelgiji imeipa Facebook saa 48 kukoma kuwadukua watu ambao hawajajiunga na mtandao huo wa kijamii.
Facebook imesema kuwa itakata rufaa uamuzi huo.
Kampuni hiyo ya mtandao wa kijamii inadai kuwa mahakama hiyo imetoa kauli hiyo kwa sababu ya programu ambayo imekuwa ikiitumia nchini humo kwa kipindi cha miaka 5 sasa.
Programmu hiyo inajipachika kwa simu ya mtu aliyeingia kwenye mtandao huo wa Facebook pale hata kama sio hajajiunga na mtandao huo wa kijamii.
Hata hivyo mahakama hiyo Ubelgiji imesema uwa Facebook haina ruhusa ya kuwadakua watu ambao sio watumizi wa mtandao wake.
Na kama watataka kuwadukua, sharti wapate idhini ya mahakama.
Image copyright PA
Image caption Iwapo Facebook itakataa kutii amri hiyo itatozwa faini ya Euro 250,000 kwa siku.
''Mahakama imeamua kuwa habari za kibinafsi zinazokusanywa na Facebook ni kinyume cha sheria na hivyo lazima Facebook iwaombe ruhusa watumizi wake ilikuafikiana na sheria za Ubelgiji,'' taarifa hiyo ilisema.
Iwapo Facebook itakataa kutii amri hiyo itatozwa faini ya Euro 250,000 kwa siku.
Programu hiyo aina ya Cookies inapigamsasa mtumiaji wa Facebook ilikubaini kama yeye ama mashine anayoitumia imewahi kutumika kujiunga na mtandao huo wa Facebook.
Msemaji wa Facebook alisema kuwa wamekuwa wakitumia programu hiyo ya Datr kwa zaidi ya miaka 5 na hiyo ndio imekuwa ikisaidia kuhakikisha akaunti za watu bilioni moja u nusu iko salama.

Mali: Miili ya watu 18 imedaiwa kupatikana hotelini

                          Polisi wa Mali wameingia katika hoteli hiyo

Maafisa wa serikali ya Mali wamesema sasa hakuna mateka wowote waliosalia katika hoteli ya Radisson Blu mjini Bamako iliyokuwa imeshambulia asubuhi na watu wenye silaha huku miili ya watu 18 ikidaiwa kupatikana ndani ya hoteli hiyo.
Waziri wa usalama wa Mali Salif Traore ameambia kikao cha wanahabari kwamba watu wenye silaha walioshambulia hoteli ya Radisson kwa sasa hawazuilii mateka wowote.
Afisi ya rais wa Mali imeandika kwenye Twitter ikishukuru maafisa wa usalama na mataifa yaliyosaidia kukabiliana na shambulio hoteli hiyo ya kifahari.
Watu watatu wamethibitishwa kufariki na wanajeshi wawili kujeruhiwa.
Ubelgiji imesema afisa mmoja wa serikali yake ni miongoni mwa waliouawa kwenye shambulio hilo.
Geoffrey Dieudonne alikuwa Mali kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa serikali.
Uvamizi huo wa wanamgambo hao ulitekelezwa mapema asubuhi kwenye hoteli hiyo ya kifahari ambayo hupendwa sana na raia wa mataifa ya nje.

Watano kuwania tuzo ya mwanasoka bora Afrika 2015

Wagombea watano wa tuzo ya BBC kwa mwanasoka bora wa mwaka 2015 wametangazwa kwenye hafla maalum iliyoandaliwa mjini Johannesburg, Afrika Kusini.
Mshindi wa tuzo la mwaka 2014 Yacine Brahimi, yupo kwenye orodha hiyo pamoja na Pierre-Emerick Aubameyang, Andrรฉ Ayew, kutoka Ghana, Sadio Manรฉ na Yaya wote wa Ivory Coast.
Mshindi ataamuliwa na mashabiki wa soka Afrika ambao watapewa fursa kupiga kura hadi tarehe 30, Novemba.
Unaweza kupiga kura mtandaoni kwa kubofya hapa au kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu kwa nambari +44 7786 20 20 08:
  • Ujumbe 1 kwa-Emerick Aubameyang
  • Ujumbe 2 kwa Andrรฉ Ayew
  • Ujumbe 3 kwa Yacine Brahimi
  • Ujumbe 4 kwa Sadio Manรฉ
  • Ujumbe 5 kwa Yaya Tourรฉ
Gharama za matumizi ya simu za kimataifa itatumika, tafadhali wasiliana na mtoa huduma wako. Ujumbe moja utatumika kwa nambari moja ya simu pekee.
Mshindi atatangazwa ijumaa tarehe 11 mwezi December wakati wa matangazo maalum kwenye BBC World News na BBC World Service, wakati mitandao ya BBC Sport na BBC Africa ikitoa pia matangazo. Kwa sheria na masharti bofya hapa.
Wagombea wa tatu mwaka huu waliopigiwa kura na wanahabari 46 kutoka Afrika wamewahi kushinda tuzo hilo: Ayew (2011), Tourรฉ (2013) na Brahimi (2014).
Aubameyang ameorodheshwa kwa mwaka wa tatu mfululizo wakati Manรฉ akijumuishwa kwa mara ya kwanza.
Mshambulizi Aubameyang amenawiri katika ufungaji magoli mwaka huu, akimaliza kama mfungaji mabao bora wa Borussia Dortmund msimu uliopita kabla ya kuandikisha rekodi mpya ujerumani kati ya 2015-16.
Mwezi Oktoba raia huyo wa Gabon, mwenye umri wa miaka 26,alikuwa mtu wa kwanza kufunga bao katika mechi nane za mwanzo katika Bundesliga huku mechi zake 17 za mashindani zikiishia ushindi mkubwa wa mabao 20 .
Mwaka huu pia umeshuhudia mafanikio makubwa kwa Ayew na ingawa haikuwa kilele, kombe la mataifa barani Afrika yalipunguza machozi yake huku the Black Stars ikishindwa na Ivory Coast.
Alikuwa na ushawishi mkubwa katika kampeni ya Ghana na kisha kuuhamisha ufanisi wake katika ligi guu ambako alifunga mabao matano katika mechi kumi alizochezea Swansea City.
Brahimi anayeichezea FC Porto amekuwa mchezaji anayelengwa barani Afrika na ulaya lakini raia huyo wa Algeria, 25, amekuwa akiongeza mabao katika ufanisi wake kwa kufunga jumla ya magoli 13 msimu uliopita huku akiisaidia klabu yake kushiriki robo fainali za ligi ya mabingwa kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka sita
Mojawepo wa mafanikio yake makubwa yalikuwa katika shindano hilo msimu uliopita ambako chenga chenga zake zingefananishwa tu na Eden Hazard wa Chelsea au nyota wa Barcelona Lionel Messi.
Tarehe 16 Mei, Mane anayeichezea Southampton alihitaji tu sekunde 176 kufunga hattrick ya haraka zaidi katika hisoria yake ya kucheza katika Premier League.
Ni miongoni mwa mabao yake 10 katika mechi 29 za Ligi ya Premia mwaka huu, matokeo yaliyoimarishwa zaidi hasa ikizingatiwa yeye ni mchezaji wa kiungo cha kati.
Mchezaji wa pekee katika orodha hii aliyewahi kunyakuwa kombe ni Tourรฉ na ilikuwa zawadi kubwa iliyoje wakati alipoiongoza Ivory Coast kunyakuwa taji la kwanza katika michuano ya kombe la mataifa katika kipindi cha zaidi ya miongo miwili.
Akiwa ndiye mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi kuwaliko wapinzani wake, mchezaji huyo wa kiungo cha kati ni mhimili katika matumaini ya klabu ya Manchester City kunyakuwa mataji na kazi yake imetambuliwa na Fifa ambayo imemteuwa kama mchezaji wa pekee kutoka Afrika kuania taji la kifahari la Ballon d’Or.












Visa vipya vya ebola vyatangazwa Liberia











 Maafisa wa afya wa Umoja wa Mataifa wanasema kumetokea maambukizi mapya ya Ebola nchini Liberia chini ya miezi mitatu baada ya nchi hiyo kutangazwa kutokuwa na ugonjwa huo.
Mgonjwa wa sasa ni mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka kumi kutoka viungani mwa mji wa, Monrovia.
Wachambuzi wanasema habari hii ni pigo kubwa kwa nchi ya Liberia ambayo imeshuhudia zaidi ya maambukizi elfu kumi na vifo zaidi ya elfu nne tangu ugonjwa wa Ebola kugunduliwa nchini humo.

Mbwa ‘shujaa wa Paris’ avuma mtandaoni

Katika vita, huwa kuna watu wanaoibuka mashujaa na kuenziwa na watu na taifa kwa jumla.
Huko Ufaransa, kuna mbwa mmoja wa polisi ambaye amepata umaarufu mkubwa sana na kusifiwa baada yake kufariki kwenye operesheni ya polisi.
Mbwa huyo wa jina Diesel anaweza kuelezwa kuwa ‘afisa wa polisi’ wa kwanza kufa vitani katika operesheni dhidi ya washukiwa walioshambulia Paris Ijumaa.

Ufaransa yawaua wapiganaji 33 Syria


                                     wapiganaji wa islamic state mjini Raqqa 

Mashambulio ya Ufaransa na mataifa mengine dhidi ya ngome ya Islamic State huko Raqqa nchini Syria siku ya jumapili yamewauwa takriban wapiganaji 33,wanaharakati wamesema.
Kundi la wapiganaji wa haki za kibinaadamu kutoka Syria limesema kuwa wengi walifariki wakati vituo vya kukagua watu vilivyoshambuliwa.



                            Ndege za kijeshi za Ufaransa zashambulia mji wa Raqqa 

Pia limeripoti kwamba familia za viongozi wa Islamic State zimeanza kuondoka Raqqa na kuelekea katika ngome nyengine ya kundi hilo katika mji wa Iraq wa Mosul.
Hatahivyo chombo kimoja cha habari kinachohusishwa na IS kimesema kuwa hakuna majeraha yoyote yaliotekelezwa na mashambulio hayo.



                              Wapiganaji wa islamic state
Kituo hicho cha Aqama kilisema siku ya jumatatu na jumanne kwamba ndege za Ufaransa zililenga ''maeneo yasio na watu,huku kundi hilo likidai kuwa lina ulinzi wa kutosha''
Kundi hilo la haki za kibinaadamu nchini Syria ambalo lina wanahabari wake nchini humo,limesema kuwa wapiganaji 33 waliaminika kuuawa katika mashambulio hayo,lakini miili yao iliharibiwa vibaya hali ya kuwa haiwezi kutambulika na hivyobasi haliwezi kutoa idadi sawa ya waliouwawa.

Tuesday, November 17, 2015










                            Mechi 14 za kufuzu kwa kombe la dunia leo 


Mechi 14 za mkondo wa pili wa kufuzu kwa fainali za kombe la dunia la mwaka wa 2018 nchini Urusi zinachezwa leo kote barani Afrika
Washindi katika mechi hizi ndio watakaofuzu kwa mkondo ujao na kujiunga na Uganda ambao tayari walijikatia tikiti baada ya kushinda Togo kwa jumla ya mabao 4-0.
Uganda, DR Congo, Morocco, Guinea na Gabon zilifuzu kusonga mbele katika hatua ya makundi baada ya kushinda mechi zao.
Gabon nao wakasonga mbele katika hatua ya makundi kwa ushindi wa mikwaju ya penalti 4-3 dhidi ya Msumbiji.
Nao Zambia, wakawachapa Sudan kwa 2-0 na kufuzu kwa makundi kwa jumla ya mabao 3-0 .
DR Congo walitoka sare ya 2-2 na Burundi huko kwao lakini wamesonga mbele baada ya kushinda mchezo wa kwanza kwa mabao 3-2 huko Bujumbura.
Morocco nao wamefuzu licha ya kufungwa 1-0 jana na Equatorial Guinea baada ya wao kushinda mechi ya kwanza 2-0.
Ratiba ya mechi za leo:
Rwanda v Libya 16:30 (0-1)
Cameroon v Niger 17:00 (3-0)
Ghana v Comoros 18:00 (0-0)
Nigeria v Swaziland 18:00 (0-0)
Congo v Ethiopia 18:00 (4-3)
Misri v Chad 19:30 (0-1)
Tunisia v Mauritania 20:00 (2-1)
Afrika Kusini v Angola 20:00 (3-1)
Ivory Coast v Liberia 20:00 (1-0)
Burkina Faso v Benin 21:00 (1-2)
Algeria v Tanzania 21:15 (2-2)
Mali v Botswana 22:00 (1-2)
Cape Verde v Kenya 22:00 (0-1)
Senegal v Madagascar 22:00 (2-2)

Bunge la Tanzania lapata spika mpya


                                      BUNGE LA TANZANIA

Job Ole Ndugai ndie spika mpya wa bunge la Tanzania. Ndugai mwenye umri wa miaka 55 alijipatia thuluthi mbili ya kura zinazohitajika.

Alikuwa naibu wa spika wa bunge lililokamilika.

Ndugai anatarajiwa kuliongoza bunge lenye zaidi ya wabunge 100 kutoka upinzani ,ikiwa ndio idadi kubwa zaidi kuwahi kuchaguliwa katika bunge hilo.

Kulikuwa na wagombea 8 waliowania wadhfa huo wa spika,lakini mwishowe ushindani ulikuwa kati ya mgombea wa chama tawala cha CCM Job Ole Ndugai na mwenzake wa upinzani Goodluck Ole Medeye kutoka chama cha Chadema.

Bunge jipya litakuwa na wanachama 394,ikiwa linawawakalishi 30 zaidi ikilinganishwa na bunge lililopita kufuatia kubuniwa kwa maeneo mapya ya ubunge.

Sunday, November 15, 2015

The best hidden features in Windows 10's major update


Microsoft's first major Windows 10 update debuted yesterday with some new features and changes. Most of the additions are obvious, but there are a few hidden away. Here are several Windows 10 features you might not have discovered yet.
Find my device
You're probably used to using a find my device feature on your phone, but what happens if you lose your laptop? In most versions of Windows you'd have to settle for a third-party app to trust and track your laptop's location, but Microsoft has decided to add this functionality straight into Windows 10. Just like the mobile equivalent, you can enable find my device and it will track the last known location of your laptop or PC.
It's linked to your Microsoft Account so you can sign-in on the web from another device if you lose your laptop or it gets stolen. You can find the setting to enable it in settings > update & security > find my device.
Cortana will let you reply to texts and more
If you have a Windows Phone then Cortana gets a lot more useful with the latest Windows 10 update. A new option in Cortana's settings section lets you enable missed call notifications. That's useful if you simply miss a call, but it also lets you reply to calls with text messages. Cortana will use your phone and its number to send the text, and you can even say "text Joe Bloggs" to initiate a text message without having to miss a call.
Sadly this isn't available yet in the new Messaging app, so you need to use Cortana at the moment to send text messages. If you have a device with a stylus then Cortana will also let you create reminders based on times, dates, and locations that you scribble into digital notes. If you're an Uber user then you can even link your account so Cortana will offer driving directions for events alongside an option to request an Uber ride.
Cortana texts
Automatic time zones
Windows has had the ability to set automatic time for years, but if you travel to another country it never changed time zones automatically. That's changing with the latest Windows 10 update. Hidden away in settings > time & language is a new "set time zone automatically" option. It's enabled by default if you install the latest update, and it does exactly what it says. Now if you're travelling for vacation or work, you won't get to your destination and be puzzled by your old time zone. It will finally work just like your smartphone does.
Cast media to device
Microsoft already supports DLNA and Miracast streaming inside Windows 10, but the latest update makes it a lot more discoverable. If you're using Microsoft Edge then there's a new option to "cast media to device" and elsewhere there's a little cast icon in apps like photos or videos. The cast media feature lets you send photos, video, and audio to compatible devices with no setup required. It's a lot like Google's Chromecast feature now.
Cast media Windows 10
Microsoft Edge sync passwords and favorites
It's surprising that password, favorites, and reading list sync wasn't enabled for the Microsoft Edge browser in Windows 10, but that's changing with the new update. If you use multiple Windows 10 devices then you can enable the sync option in Edge settings so the browser finally syncs passwords and favorites across all the laptops and PCs you use.
New Skype apps
Microsoft is including Skype integration with its latest Windows 10 update, but you might not even notice it at first. If you install the latest update then apps like Messaging, Phone, and Skype Video will also be installed. You can find them using Cortana or the app list, and they're basic versions of Skype features. They're useful if you want a lightweight messaging app to talk to Skype friends, but they still need some improvements.
Windows 10 Skype integration
Better app snapping
Windows 8 introduced some useful "Metro" app snapping features, and now Windows 10 is extending them to all apps. When you place two desktop apps side-by-side, like File Explorer and Notepad, you can now resize them individually and the other window will adjust to fill the gap. It's a lot more like how Metro-style apps worked in Windows 8, and it's great if you want to have apps side-by-side but have one act like it's a sidebar. Just hover your mouse in the middle of two snapped apps and you'll see a new slider will appear to let you adjust accordingly.

Mshambulizi Paris atajwa:Omar Mostefai


Waendesha mashtaka wanaouchunguza matukio ya mashambulio ya kigaidi mjini Paris Ufaransa wamemtaja mmoja wa washambuliaji 7 wa kujitoa mhanga.

Omar Ismail Mostefai mwenye umri wa miaka 29 anasemekana kuwa ni raia wa ufaransa aliyekuwa anachunguzwa na polisi wa kupamabana na ugadi kabla hajatoweka.
Mtu huyo tayari alikuwa na rekodi ya uhalifu.
Omar ametambuliwa kutokana na kidole kilichopatikana katika eneo la tukio.



Kiongozi wa mashtaka wa Ufaransa Francois Molins 

  Uchunguzi pia utalenga kubaini iwapo aliwahi kusafiri kwenda Syria au la .
Wachunguzi hao wanasema washambuliaji hao walijipanga katika vikundi vitatu kabla ya kutekeleza mashambulizi hayo kwa mabomu na ufyatuaji wa risasi.

Mbali na bunduki washabuliaji hao pia walikuwa na mikanda ya mabomu waliotumia kujilipua katika msururu huo wa mashambulio yaliyosababisha vifo vya watu 129.

Wengi wa waliolengwa walikuwa mashabiki wa tamasha la muziki, wateja katika migahawa ,baa na hata mashabiki wa soka.
Kundi la wanamgambo wa I S wamedai kuhusika na tukio hilo.
Rais wa Ufaransa ametangaza hali ya hatari na kufunga kabisa mipaka ya taifa hilo.
Washambuliaji 7 walijilipua huku mmoja wao akipigwa risasi wakati wa operesheni ya kuokoa maisha ya watu waliokuwa ndani ya ukumbi huo wa maonyesho.

Wachunguzi wanasema kuwa wanahofu kuwa washambulizi zaidi waliotoroka na sasa msako unaendelea.
Rais wa Ufaransa ametangaza hali ya hatari na kufunga kabisa mipaka ya taifa hilo.


Halima Mdee Atoa Kauli Nzito Kuhusu Mauaji wa Mwenyekiti wa Chadema Geita Aliye Uawa Kwa Ajili ya Siasa


Watu Mbali mbali Wameguswa na Kifo cha Kamanda wa Chadema Mawazo Ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Geita...
Hapa chini Nimekuwekea ujumbe kutoka kwa Halima Mdee aliondika mtandaoni:


"Ameuwawa Kwa Sababu tu ya Uchaguzi wa Kata!!! Damu yake Haitapotea BURE!!! Ipo siku, Wanyonge Watanyanyuka" Halima James Mdee

Mkwasa Afunguka: Tulifanya Kosa Kubwa Sana Kufanya Mabadiliko Wakati Timu ilikuwa Vizuri na Stable......


Baada ya timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Star’ kulazimishwa sare ya kufungana magoli 2-2 na Algeria kwenye uwanja wa taifa, kocha mkuu wa kikosi hicho Charles Boniface Mkwasa amesema, mabadiliko yaliyofanywa na benchi la ufundi kumtoa Elius Maguli na kumingiza Mrisho Ngassa hayakuzaa matunda kama walivyotarajia.

Mkwasa amesema, walimuanziasha Maguli kwasababu ni mchezaji ambaye anatumia nguvu na anaweza kupambana kwa kutumia mwili wake lakini baadaye walimpumzisha wakiamini kuingia kwa Ngassa kungeifanya timu kutengeneza  nafasi nyingi zaidi za kufunga kwasanbabu Ngassa anaspidi na uwezo wa kutengeneza nafasi.

“Niseme tu kwamba leo (jana) ilikuwa ni game yetu 100%  tumetengeneza nafasi nyingi sana lakini tumeshindwa kuzitumia tumepata goli mbili lakini kuna muda tumepoteza concentration wakaweza kurudisha goli zote mbili lakini vijana wamepambana wamehangaika kutafuta magoli kutokana na nafaisi zilizopatikana na wakati mwingine tunasema mpira unabahati na Algeria wanabahati sana”, alisema Mkwasa.

“Vijana wamejitahidi lakini niseme tulifanya makosa pengine wakati wa kufanya mabadiliko kwasababu timu ilishakuwa stable lakini ni matokeo ya mchezo na nafikiri bado tunamlima mrefu kwasababu ninavyowatazama hawa nyumbani kwao watabadilika. Lakini uwezo wa kuwafunga tunao timu yao sio nzuri sana kiasi kwamba haifungiki”.

“Niwashukuru watanzania na waandishi wa habari kwa kuhamasisha na watanzania wameweza kuitikia na tumeona jinsi gani wameishangilia timu yao lakini wasife moyo kwa matokeo haya, tupo katika mchakato wa kujenga timu naamini katika muda mfupi tutakuwa na timu nzuri kama wenzetu ambavyo wanatimu zao”.

“Niwashukuru pia wachezaji na wengine wote ambao tumeshirikiana, kamati pamoja na TFF kwa kuweza kuonesha kiwango ambacho kwa muda mrefu hakijaonekana”.

Kikosi cha Stars kimeondoka jana usiku kuelekea nchini Algeria kwa ajili ya mchezo wa marudiano utakaopigwa Jumanne November 17.