Saturday, May 28, 2016

"Worlds Brightest" Military Grade Flashlight Now Available To Public







 





get video





The important functions of a supervisor are:


Tuesday, May 24, 2016

Helikopta na malori ya Urusi yateketea Syria

By on 11:55:00 AM

 Helikopta 4 na malori 20 ya Urusi yateketea nchini Syria


Picha za satellite zilitolewa kwa BBC zinaonyesha kuwa ndege nne za Urusi aina ya helkopta na malori 20 viliteketea moto ndani ya kambi moja ya kijeshi iliyo kati kati mwa Syria wiki iliyopita.
Kampuni moja ya ujasusi ya Marekani, Stratfor, iliyotoa picha hizo, inasema kuwa kuna uwezekano mkubwa kuwa Islamic State walihusika na uharibifu huo.
Islamic state hawajasema kuwa ni wao walihusika lakini taarifa kutoka kwa kundi hilo zinasema kuwa helikopta na malori yaliteketea.
Baadhi ya wataalamu wanasema kuwa huenda moto ulisambaa kutoka kwa tangi la mafuta ambalo lilipuka. Urusi bado haijazungumzia kisa hicho.

Uganda yailalamikia DRC kwa vifo vya polisi wake

By on 11:47:00 AM
 Afisa mkuu wa Polisi nchini Uganda Edward Kayihura




Serikali ya Uganda imewasilisha ombi rasmi kwa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo baada ya maafisa wanne wa Uganda kupigwa risasi katika Ziwa Albert,ambalo linagawanya mpaka wa mataifa hayo mawili kulingana na chombo cha habari cha AFP.
Wanne hao waliuawa wakati walipokuwa wakichunguza uvuvi haramu unaotekelezwa katika ziwa hilo.
AFP ilimnukuu waziri wa maswala ya kigeni Henry Okello Oryem akisema kuwa maafisa hao wanne walikuwa kazini katika eneo la Uganda.
''Waliuawa wakiwa kazini na miili yao kuchukuliwa na mamlaka ya DRC.Tumeweka wazi,katika siku za usoni visa kama hivi vitaishinikiza Uganda kujilinda ikiwemo kuwatafuta wahusika''.

Boti iliyopata ajali Ziwa Nyasa yatafutwa

By on 11:44:00 AM
Boti iliyofanya safari kutoka Mbamba Bay inahofiwa kupigwa dhoruba





Takriban watu 12 hawajulikani walipo hadi sasa, wakihofiwa kufa maji baada ya boti iliyokuwa ikifanya safari kutoka Mbamba Bay nchini Tanzania kwenda Nkhata Bay Malawi kuzama kwenye Ziwa Nyasa.
Duru za usalama zinasema Boti hiyo haijulikani ilipo wala abiria waliokuwemo ndani yake.
Kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma, kusini mwa Tanzania, Zuberi Mwombeji amesema haifahamiki ajali hiyo ilitokea aneo gani la Ziwa.
''Usafiri wa kutoka Mbamba Bay mpaka Nkhata Bay huchukua saa tano mpaka sita, walipoona Nkhata Bay hawajafika waliwasiliana na watu wa Mbamba Bay ndipo ilipojulikana kuwa kuna tatizo limetokea'' alieleza Kamanda Mwombeji.
Chanzo cha ajali hiyo kimeelezwa kuwa hali mbaya ya hewa ziwani, hali inayoaminika kuwa ilisababisha Boti hiyo kupigwa dhoruba.
Shughuli za kuisaka Boti iliyotoweka zinaendelea.

Wednesday, May 18, 2016

Utata wazuka kuhusu msichana wa Chibok
















Kuna utata kuhusu ni nani alimuokoa na jina la msichana ni lipi.
 
Kumezuka utata kuhusu msichana wa Chibok ambaye aliokolewa nchini Nigeria. Kwanza jeshi linasema kuwa ndilo lilimuokoa msichana huyo aliyetjwa jina kuwa Falmata Mbalala.
Hata hivyo wanaharakati na viongozi wa kijamii wanasema kuwa msichana aliyeokolewa, jina lake ni Amina Ali Nkek na kuwa alipatikana katika msitu wa Sambisa na kundi la vijana na kudumisha usalama.
Msitu huo ndio maficho makuu ya wanamgambo wa Boko Haram.
Mwenyeki wa chama cha wazazi wa Cibok mjini Abuja Hosea Abana Tsambido aliiambia BBC kuwa vijana hao walikuwa na habati kubwa kumpata msichana huyo.

Msichana wa Chibok kukutana na Rais Buhari

Dakika 59 zilizopita Mshirikishe mwenzako

 https://www.blogger.com/blogger.g?blogID=6465176323126612680#editor/target=post;postID=3977667580274640770
 
 
 Msemaji wa Serikali ya Nigeria amesema msichana kutoka Chibok, aliyeokolewa hivi karibuni kutoka mikononi mwa Wanamgambo wa Boko Haram, atakutana na Rais Muhammadu Buhari na kupata msaada wa kuweza kuchangamana na jamii yake.
Aliachiwa huru akiwa na mtoto mchanga, hili ni tukio la uokoaji la kwanza kwa kipindi cha zaidi ya miaka miwili..
Zaidi ya wasichana mia mbili walitekwa na kundi hilo la Boko haram mwezi April mwaka 2014.
Jeshi la Nigeria limesema tayari limeshamkamata mfuasi wa Boko Haram ambaye inasemakana na mume wa msichana huyo. Zaidi ya wasichana mia mbili walitekwa na kundi hilo la Boko haram mwezi April mwaka 2014.
Msemaji wa serikali ya Nigeria Garba Shehu ameiambia BBC kuwa msichana huyo wa Chibok, aliyeokolewa hivi karibuni kutoka katika mikono Boko haramu atakutana na Rais Muhammadu Buhari na atapewa msaada na serikali ili aweze kurejea katika jamii.
Naye Aboku Gaji ambaye ni kiongozi wa kikundi cha wanamgambo ambaye alimuokoa binti huyo na kuiambia BBC juu ya namna familia yake ilivyompokea aliporudishwa nyumbani.

Saturday, May 14, 2016

Yajue maudhi kumi (10) YA kompyuta


1. Hazifanyi kazi hadi zichajiwe au ziunganishwe kwenye umeme.
2. Zinaweza kuzima ghafla na kukupotezea kazi ambayo hukuisevu.
3. Kompyuta humfanya mtu awe “addicted” kila muda ukiona kompyuta mikono inakuwasha.
4. Kompyuta hubadilika haraka kimatumizi na kiumbo. Kila siku  zinatolewa aina mpya, hivyo utajikuta unatumia kompyuta ambayo ishapitwa  na wakati.
5. Matatizo ya programu, programu huuzwa tofauti na kompyuta kwahiyo kila kitu unanunua hupewi pamoja na kompyuta.
6. Tatizo la vifaa, ni gharama sana kununua kifaa kama kimeharibika kwenye kompyuta yako.
7. Kompyuta huharibika haraka sana, inahitaji matunzo makubwa ili kuinusuru.
8. Virusi, kompyuta huhathiliwa sana na virusi na kukufanya uweze kupoteza nyaraka zako muhimu katika kompyuta.
9. Kompyuta huhitaji kubadilishwa mara kwa mara kwani kila siku  zinatoka aina mpya. Hii itakusababisha kuingia gharama mara kwa mara.
10. Kompyuta huzidisha kazi kwani kama wewe ni mfanyakazi utahitajika  ujibu “email” za bosi wako hata ukiwa nyumbani tofauti na zamani..

-

Friday, May 13, 2016

Mwanamke wa Senegal ateuliwa katibu mkuu Fifa


Samoura
Add caption

Ni mara ya kwanza mwanamke kuteuliwa katibu mkuu Fifa
Kwa mara ya kwanza katika historia, mwanamke ameteuliwa kuwa katibu mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), shirikisho ambalo kwa kiwango kikubwa limetawaliwa na wanaume.
Bi Fatma Samba Diouf Samoura kutoka Senegal, ndiye katibu mkuu mpya.
Atasimamia shughuli za kila siku katika shirikisho hilo ambalo kwa kipindi cha mwaka mmoja sasa limekabiliwa na tuhuma za ulaji rushwa.
Ni mwanadiplomasia aliyehitimu ambaye kwa sasa amekuwa akihudumu kama mratibu wa masuala ya kibinadamu katika Umoja wa Mataifa nchini Nigeria.
Amefanya kazi UN kwa miaka 21.
Bi Samoura amesema ni fahari kubwa sana kwake kuteuliwa kwenye wadhifa huo.
Tangazo hilo limefanywa na rais wa FIFA Gianna Infantino katika kongamano kuu la FIFA linaloendelea Mexico.
Aliyekuwa katibu mkuu wa FIFA Jerome Valcke alipigwa marufuku kutojihusisha na shughuli zozote za soka kwa miaka 12 mapema mwaka huu.



















Mwanamume 'adandia' helikopta Bungoma Kenya

By on 12:57:00 PM
Ndege
Ndege hiyo ilipaa na kuondoka naye
Mwanamume mmoja katika mji wa Bungoma, Magharibi mwa Kenya ameshangaza wengi baada ya kudandia helikopta ambayo imepaa na kuondoka naye.
Helikopta hiyo ilikuwa imesafirisha mwili wa mfanyabiashara mashuhuri Jacob Juma aliyeuawa kwa kupigwa risasi jijini Nairobi wiki iliyopita, vyombo vya habari nchini Kenya vinasema.
Video zinazosambaa mtandaoni zinaonesha helikopta hiyo ikipaa juu angani kutoka uwanja wa Posta, mwanamume huyo akiwa amejishikilia kwenye vyuma vya helikopta hiyo.
Taarifa zinasema baadaye ndege imetua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Bungoma na mwanamume huyo akapelekwa hospitalini.
Kitambulisha mada #Bungoma kimeanza kuvuma kwenye Twitter nchini Kenya, watu wakijadili tukio hilo.
Wengi wameeleza kushangazwa kwao na wengine wanalifanyia mzaha.
Baadhi wanasema mwanamume huyo alisahau leo ilikuwa Ijumaa tarehe 13, ambayo kwa baadhi ni siku yenye kutokea mabaya.Wengine wanatumia majina ya filamu na hata nyimbo. Mfano wimbo wa 'I Believe I Can Fly', wake R Kelly na filamu ya Mission: Impossible ambayo mwigizaji nyota wake ni Tom Cruise.https://www.blogger.com/blogger.g?blogID=6465176323126612680#editor/target=post;postID=2149767923202216375

Monday, May 9, 2016

Malkia wa Pembe' afikishwa kortini Tanzania

By on 12:31:00 PM



Malkia wa Pembe kutoka China Kesi dhidi ya mwanamke mfanyabiashara raia wa China anayetuhumiwa na mashtaka ya kuendeleza mtandaoa wa kihalifu wa ulanguzi wa pembe barani Asia imeahirishwa kwa wiki mbili nchini Tanzania.
Alifikishwa mahakamani Jumatatu asubuhi mjini Dar es Salaam.
Waendesha mashtaka wanasema Yang Feng Glan, anayejulikana kwa umaarufu pia kama Malkia wa pembe, aliendesha biashara haramu ya kuwaua ndovu katika mbuga za wanyama ili kupata pembe zao ambazo wanazisafirisha na kuziuza katika mataifa ya bara Asia.
Anashutumiwa kwa kuendeleza shughuli hiyo kwa takriban miaka 14.
Anakana mashtaka hayo.
Mahakama imeambiwa kwamba faili ya kesi yake bado imo mikononi mwa mkurugenzi wa mashtaka ya umma.
Maafisa wa serikali Tanzania walitaja kukamatwa kwa Yang Feng Glan mnamo Oktoba mwaka jana kama ufanisi mkubwa.
Taifa hilo la Afrika mashariki limepoteza thuluthi mbili za ndovu wake katika kipindi cha miaka kumi iliyopita

Jumba la ghorofa laporomoka Mombasa

By on 12:17:00 PM





 
Maafisa wa serikali wamefika eneo hilo
Sehemu ya jumba kubwa la kibiashara mjini Mombasa imeporomoka siku chache baada ya jumba la makazi kuporomoka jijini Nairobi na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 40.
Sehemu ya jumba hilo la Nyali Centre, yenye ghorofa sita, iliporomoka usiku wa kuamkia Jumatatu.
Hakuna aliyeripotiwa kujeruhiwa wakati wa mkasa huo.
Jumba la Nyali Centre huwa na kituo cha mazoezi na mgahawa maarufu.
Waziri wa serikali ya jimbo la Mombasa Francis Thoya amesema jumba hilo litachunguzwa kubaini iwapo ni thabiti.
“Nadhani sehemu ambapo vyoo hivyo vilifaa kuuunganishwa na jumba lenyewe ndiyo ilikuwa na shida. Ninamsaka mhandisi na aliyepewa kandarasi,” amesema.
“Lakini unapopata visa kama hivi, ni ishara tosha kuwa inafaa tuchunguze upya mijengo yetu. Kwa hivyo kutakuwa na ukaguzi wa baadhi ya mijengo mikuu ambayo inatumiwa na umma.”



 

 Maafisa wa serikali wamefika eneo hilo
Sehemu ya jumba kubwa la kibiashara mjini Mombasa imeporomoka siku chache baada ya jumba la makazi kuporomoka jijini Nairobi na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 40.
Sehemu ya jumba hilo la Nyali Centre, yenye ghorofa sita, iliporomoka usiku wa kuamkia Jumatatu.
Hakuna aliyeripotiwa kujeruhiwa wakati wa mkasa huo.
 
Jumba la Nyali Centre huwa na kituo cha mazoezi na mgahawa maarufu.
Waziri wa serikali ya jimbo la Mombasa Francis Thoya amesema jumba hilo litachunguzwa kubaini iwapo ni thabiti.
“Nadhani sehemu ambapo vyoo hivyo vilifaa kuuunganishwa na jumba lenyewe ndiyo ilikuwa na shida. Ninamsaka mhandisi na aliyepewa kandarasi,” amesema.
“Lakini unapopata visa kama hivi, ni ishara tosha kuwa inafaa tuchunguze upya mijengo yetu. Kwa hivyo kutakuwa na ukaguzi wa baadhi ya mijengo mikuu ambayo inatumiwa na umma.”

Magufuli aahidi sukari ya bei ya chini

By on 12:09:00 AM




 


Serikali ya Tanzania imeagiza sukari ilikukabiliana na upungufu wa sukari uliopo nchini.
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amesema badala ya kuwapa wafanyabiashara leseni ya kuagiza sukari kutoka ng'ambo serikali yenyewe ndio itaagiza sukari hiyo moja kwa moja.
Kauli hiyo inawadia baada ya mabohari zaidi kugunduliwa kote nchini yakiwa yamejaa sukari iliyoagizwa kutoka nje na ile iliyonunuliwa kwa wingi kutoka kwenye kampuni za kusaga sukari za humohumo Tanzania.
''Kuna mmoja ambaye amepatikana Arusha amehodhi zaidi ya tani elfu tano ya sukari naye mwengine huko Kilombero amenunua sukari yote kutoka kwa kampuni za humu humu nchini na akaficha.''
''Lakini hili ni swala la sasa tu, katika siku zijazo sukari itapatikana kwa wingi hapa Tanzania.Serikali imekwisha agiza sukari lakini hatutawapa hawa waliofilisi watanzania leseni ya kuingiza tena sukari.
''Serikali imeagiza na itauza sukari hiyo kwa bei ya chini... hilo ndilo lengo la serikali '' alisema rais Magufuli huku mawananchi wakimshangilia
Katika siku zijazo sukari itapatikana kwa wingi hapa Tanzania.Serikali imekwisha agiza sukari lakini hatutawapa hawa waliofilisi watanzania leseni ya kuingiza tena sukari.''
.
 ''
Sukari hiyo ambayo huwa ni ya bei ya chini hubadilishwa na kisha kuvikwa magunia ya makampuni ya Kitanzania yanayosaga sukari na kisha kuuzwa rejareja.
Tumbua tumbua ya rais Magufuli imesadifiana na tangazo la Halmashauri ya ushuru ya Tanzania TRA kuwa imeanza kugawa sukari iliyoingizwa nchini kinyume cha sheria na kufichwa katika mabohari kote nchini.
TRA ilichukua hatua hiyo baada ya mwekezaji wa kibinafsi mkoani Lindi kupatikana na zaidi ya mifuko elfu tano za sukari kutoka nga'mbo.
Yamkini sukari hiyo hubadilishwa kwenye mifuko yenye nembo ya kampuni za kusaga sukari za Tanzania na kisha kuuzwa kwa bei maradufu.

Saturday, May 7, 2016

Naibu kamanda wa kundi la mauaji Rwanda akamatwa

  • Saa moja iliyopita
Image copyright
Image caption Mpiganaji wa kundi la FDLR
Wakuu wa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo wanasema wamemkamata naibu kamanda wa kundi la wapiganaji, linalohusishwa na mauaji makubwa ya Rwanda ya mwaka 1994.
Msemaji wa serikali, alieleza kuwa Jenerali Leopold Mujyambere, wa kundi la Rwanda la FDLR, alikamatwa mjini Goma, mashariki mwa nchi.
FDLR kisangani
 
Kundi la FDLR ni la Wahutu wanaoshutumiwa kuuwa malaki ya Watutsi na Wahutu waliokuwa na msimamo wa wastani, wakati wa mauaji ya kimbari ya Rwanda.
Rwanda imeingilia kati kijeshi mashariki mwa Congo katika juhudi za kuliangamiza kundi hilo.










downlod


DIRA YA DUNIA JUMATATU 02.05.2016

dira ya dunia







downlod