Helikopta 4 na malori 20 ya Urusi yateketea nchini Syria
Picha za satellite
zilitolewa kwa BBC zinaonyesha kuwa ndege nne za Urusi aina ya helkopta
na malori 20 viliteketea moto ndani ya kambi moja ya kijeshi iliyo kati
kati mwa Syria wiki iliyopita.
Kampuni moja ya ujasusi ya
Marekani, Stratfor, iliyotoa picha hizo, inasema kuwa kuna uwezekano
mkubwa kuwa Islamic State walihusika na uharibifu huo.
Islamic
state hawajasema kuwa ni wao walihusika lakini taarifa kutoka kwa kundi
hilo zinasema kuwa helikopta na malori yaliteketea.
Baadhi ya
wataalamu wanasema kuwa huenda moto ulisambaa kutoka kwa tangi la mafuta
ambalo lilipuka. Urusi bado haijazungumzia kisa hicho.
Serikali ya Uganda
imewasilisha ombi rasmi kwa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
baada ya maafisa wanne wa Uganda kupigwa risasi katika Ziwa
Albert,ambalo linagawanya mpaka wa mataifa hayo mawili kulingana na
chombo cha habari cha AFP.
Wanne hao waliuawa wakati walipokuwa wakichunguza uvuvi haramu unaotekelezwa katika ziwa hilo.
AFP
ilimnukuu waziri wa maswala ya kigeni Henry Okello Oryem akisema kuwa
maafisa hao wanne walikuwa kazini katika eneo la Uganda.
''Waliuawa
wakiwa kazini na miili yao kuchukuliwa na mamlaka ya DRC.Tumeweka
wazi,katika siku za usoni visa kama hivi vitaishinikiza Uganda kujilinda
ikiwemo kuwatafuta wahusika''.
Takriban watu 12
hawajulikani walipo hadi sasa, wakihofiwa kufa maji baada ya boti
iliyokuwa ikifanya safari kutoka Mbamba Bay nchini Tanzania kwenda
Nkhata Bay Malawi kuzama kwenye Ziwa Nyasa.
Duru za usalama zinasema Boti hiyo haijulikani ilipo wala abiria waliokuwemo ndani yake.
Kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma, kusini mwa Tanzania, Zuberi Mwombeji amesema haifahamiki ajali hiyo ilitokea aneo gani la Ziwa.
''Usafiri
wa kutoka Mbamba Bay mpaka Nkhata Bay huchukua saa tano mpaka sita,
walipoona Nkhata Bay hawajafika waliwasiliana na watu wa Mbamba Bay
ndipo ilipojulikana kuwa kuna tatizo limetokea'' alieleza Kamanda
Mwombeji.
Chanzo cha ajali hiyo kimeelezwa kuwa hali mbaya ya hewa ziwani, hali inayoaminika kuwa ilisababisha Boti hiyo kupigwa dhoruba.
Shughuli za kuisaka Boti iliyotoweka zinaendelea.
Kumezuka utata
kuhusu msichana wa Chibok ambaye aliokolewa nchini Nigeria. Kwanza jeshi
linasema kuwa ndilo lilimuokoa msichana huyo aliyetjwa jina kuwa
Falmata Mbalala.
Hata hivyo wanaharakati na viongozi wa kijamii
wanasema kuwa msichana aliyeokolewa, jina lake ni Amina Ali Nkek na kuwa
alipatikana katika msitu wa Sambisa na kundi la vijana na kudumisha
usalama.
Msitu huo ndio maficho makuu ya wanamgambo wa Boko Haram.
Mwenyeki
wa chama cha wazazi wa Cibok mjini Abuja Hosea Abana Tsambido aliiambia
BBC kuwa vijana hao walikuwa na habati kubwa kumpata msichana huyo.
Msemaji wa Serikali
ya Nigeria amesema msichana kutoka Chibok, aliyeokolewa hivi karibuni
kutoka mikononi mwa Wanamgambo wa Boko Haram, atakutana na Rais
Muhammadu Buhari na kupata msaada wa kuweza kuchangamana na jamii yake.
Aliachiwa huru akiwa na mtoto mchanga, hili ni tukio la uokoaji la kwanza kwa kipindi cha zaidi ya miaka miwili..
Zaidi ya wasichana mia mbili walitekwa na kundi hilo la Boko haram mwezi April mwaka 2014.
Jeshi
la Nigeria limesema tayari limeshamkamata mfuasi wa Boko Haram ambaye
inasemakana na mume wa msichana huyo. Zaidi ya wasichana mia mbili
walitekwa na kundi hilo la Boko haram mwezi April mwaka 2014.
Msemaji
wa serikali ya Nigeria Garba Shehu ameiambia BBC kuwa msichana huyo wa
Chibok, aliyeokolewa hivi karibuni kutoka katika mikono Boko haramu
atakutana na Rais Muhammadu Buhari na atapewa msaada na serikali ili
aweze kurejea katika jamii.
Naye Aboku Gaji ambaye ni kiongozi wa
kikundi cha wanamgambo ambaye alimuokoa binti huyo na kuiambia BBC juu
ya namna familia yake ilivyompokea aliporudishwa nyumbani.
1. Hazifanyi kazi hadi zichajiwe au ziunganishwe kwenye umeme. 2. Zinaweza kuzima ghafla na kukupotezea kazi ambayo hukuisevu. 3. Kompyuta humfanya mtu awe “addicted” kila muda ukiona kompyuta mikono inakuwasha. 4. Kompyuta hubadilika haraka kimatumizi na kiumbo. Kila siku zinatolewa aina mpya, hivyo utajikuta unatumia kompyuta ambayo ishapitwa na wakati. 5. Matatizo ya programu, programu huuzwa tofauti na kompyuta kwahiyo kila kitu unanunua hupewi pamoja na kompyuta. 6. Tatizo la vifaa, ni gharama sana kununua kifaa kama kimeharibika kwenye kompyuta yako. 7. Kompyuta huharibika haraka sana, inahitaji matunzo makubwa ili kuinusuru. 8. Virusi, kompyuta huhathiliwa sana na virusi na kukufanya uweze kupoteza nyaraka zako muhimu katika kompyuta. 9. Kompyuta huhitaji kubadilishwa mara kwa mara kwani kila siku zinatoka aina mpya. Hii itakusababisha kuingia gharama mara kwa mara. 10. Kompyuta huzidisha kazi kwani kama wewe ni mfanyakazi utahitajika ujibu “email” za bosi wako hata ukiwa nyumbani tofauti na zamani..
Ni mara ya kwanza mwanamke kuteuliwa katibu mkuu Fifa
Kwa mara ya kwanza
katika historia, mwanamke ameteuliwa kuwa katibu mkuu wa Shirikisho la
Soka Duniani (FIFA), shirikisho ambalo kwa kiwango kikubwa limetawaliwa
na wanaume.
Bi Fatma Samba Diouf Samoura kutoka Senegal, ndiye katibu mkuu mpya.
Atasimamia
shughuli za kila siku katika shirikisho hilo ambalo kwa kipindi cha
mwaka mmoja sasa limekabiliwa na tuhuma za ulaji rushwa.
Ni
mwanadiplomasia aliyehitimu ambaye kwa sasa amekuwa akihudumu kama
mratibu wa masuala ya kibinadamu katika Umoja wa Mataifa nchini Nigeria.
Amefanya kazi UN kwa miaka 21.
Bi Samoura amesema ni fahari kubwa sana kwake kuteuliwa kwenye wadhifa huo.
Tangazo hilo limefanywa na rais wa FIFA Gianna Infantino katika kongamano kuu la FIFA linaloendelea Mexico.
Aliyekuwa
katibu mkuu wa FIFA Jerome Valcke alipigwa marufuku kutojihusisha na
shughuli zozote za soka kwa miaka 12 mapema mwaka huu.
Mwanamume mmoja
katika mji wa Bungoma, Magharibi mwa Kenya ameshangaza wengi baada ya
kudandia helikopta ambayo imepaa na kuondoka naye.
Helikopta hiyo
ilikuwa imesafirisha mwili wa mfanyabiashara mashuhuri Jacob Juma
aliyeuawa kwa kupigwa risasi jijini Nairobi wiki iliyopita, vyombo vya
habari nchini Kenya vinasema.
Video zinazosambaa mtandaoni
zinaonesha helikopta hiyo ikipaa juu angani kutoka uwanja wa Posta,
mwanamume huyo akiwa amejishikilia kwenye vyuma vya helikopta hiyo.
Taarifa zinasema baadaye ndege imetua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Bungoma na mwanamume huyo akapelekwa hospitalini.
Kitambulisha mada #Bungoma kimeanza kuvuma kwenye Twitter nchini Kenya, watu wakijadili tukio hilo.
Wengi wameeleza kushangazwa kwao na wengine wanalifanyia mzaha.
Baadhi wanasema mwanamume huyo alisahau leo ilikuwa Ijumaa tarehe 13, ambayo kwa baadhi ni siku yenye kutokea mabaya.Wengine wanatumia majina ya filamu na hata nyimbo. Mfano wimbo wa 'I
Believe I Can Fly', wake R Kelly na filamu ya Mission: Impossible ambayo
mwigizaji nyota wake ni Tom Cruise.https://www.blogger.com/blogger.g?blogID=6465176323126612680#editor/target=post;postID=2149767923202216375
Malkia wa Pembe kutoka China
Kesi dhidi ya mwanamke mfanyabiashara raia wa
China anayetuhumiwa na mashtaka ya kuendeleza mtandaoa wa kihalifu wa
ulanguzi wa pembe barani Asia imeahirishwa kwa wiki mbili nchini
Tanzania.
Alifikishwa mahakamani Jumatatu asubuhi mjini Dar es Salaam.
Waendesha
mashtaka wanasema Yang Feng Glan, anayejulikana kwa umaarufu pia kama
Malkia wa pembe, aliendesha biashara haramu ya kuwaua ndovu katika mbuga
za wanyama ili kupata pembe zao ambazo wanazisafirisha na kuziuza
katika mataifa ya bara Asia.
Anashutumiwa kwa kuendeleza shughuli hiyo kwa takriban miaka 14.
Anakana mashtaka hayo.
Mahakama imeambiwa kwamba faili ya kesi yake bado imo mikononi mwa mkurugenzi wa mashtaka ya umma.
Maafisa wa serikali Tanzania walitaja kukamatwa kwa Yang Feng Glan mnamo Oktoba mwaka jana kama ufanisi mkubwa.
Taifa hilo la Afrika mashariki limepoteza thuluthi mbili za ndovu wake katika kipindi cha miaka kumi iliyopita
Image copyrightImage caption
Mpiganaji wa kundi la FDLR
Wakuu wa Jamhuri ya
Demokrasi ya Congo wanasema wamemkamata naibu kamanda wa kundi la
wapiganaji, linalohusishwa na mauaji makubwa ya Rwanda ya mwaka 1994.
Msemaji
wa serikali, alieleza kuwa Jenerali Leopold Mujyambere, wa kundi la
Rwanda la FDLR, alikamatwa mjini Goma, mashariki mwa nchi.
Kundi la FDLR ni la Wahutu wanaoshutumiwa kuuwa
malaki ya Watutsi na Wahutu waliokuwa na msimamo wa wastani, wakati wa
mauaji ya kimbari ya Rwanda.
Rwanda imeingilia kati kijeshi mashariki mwa Congo katika juhudi za kuliangamiza kundi hilo.