Friday, December 11, 2015

Thursday, December 3, 2015

Well come in talanta group olasity Kati arusha Tanzania we produce good instruments for water management like ports. Tank ect

                                                     tok

kwa maelezo piga sm 0759894855

Tuesday, December 1, 2015

Marekani kutuma jeshi kushambulia IS

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Ash Carter amesema jeshi maalum la Marekani litatumwa kwenda nchini Iraq kupambana na wapiganaji wa Islamic State katika nchi za Iraq na Syria.
Amesema majeshi hayo yatafanya operesheni hiyo ikiwa ni pamoja kuwaokoa mateka na kuwakamata viongozi wa I S.
Wakati huo huo Rais wa Syria Bashar Al Assad amesema uamuzi wa Urusi kuingia vitani katika nchi yake kumedhoofisha nguvu ya wapigani wa Islamic state tofauti na majeshi ya Marekani ambayo yamefanya kundi hilo kujiimarisha zaidi.
Waziri huyo wa ulinzi wa Marekani Ash Carter alitoa kauli hiyo wakati akiongea kwenye Kamati ya Congress huko Washtong nchini Marekani.
"Kuongeza kasi hiyo tutatuma tena kwa amri ya rais Obama na kwa ushauri wa mwenyekiti na wangu, Kikosi maalum cha kijeshi nchini Syria kusaidia kupambana na wapiganaji wa ISIL. Majeshi hayo maalum ya uwezo maalum wa kufanya kazi mbali mbali. Litatusaisia kufanya upelelezi wa ardhini kusaidia majeshi ya nchi hizo na watarudisha maeneo yaliyochutekwa na ISIL. Mahali tutakapopata nafasi kuteka maeneo tutapanua harakati zaidi."
Aidha Cater amesema katika maeneo ya Iraq majeshi hayo yatapambana na vilivyo na wapiganaji wa Islamic State.
"Kwa uratibu kamili na serikali ya Iraq tutapeleka majeshi maalum kupambana kwa kusaidia majeshi ya Iraq na wapiganaji wa Peshmega kuzidi kuwashughulikia ISIL. Majeshi haya maalum kwa muda wote watakuwa na uweza wa kuendesha opesheni kuwaachia huru mateka kukusanya taarifa za kiusalama na kuwakamata viongozi wa ISIL."
Wakati huo huo Rais wa Syria Bashar Al Assad amesema uamuzi wa Urusi kuingia vitani katika nchi yake imebadilisha hali katika uwanja wa vita. Katika mahojiano kwenye kituo cha televisheni cha Czech Assad amesema tangu Urusi ilipoingilia kati kijeshi wapigani wa Islamic State na makundi mengine ya jihad yamedhoofika, na amesema anaamini msaada wa Urusi utaendelea. Amesema majeshi ya Urusi yamekuwa na uwezo na uamuzi wa hali ya juu tofauti na majeshi ya ushirika yanayoongozwa na Marekani.
Katika hatua nyingine naye Waziri Mkuu wa Uingereza amewaomba wabunge wa chama cha Conservative kuunga mkono mpango wake wa majeshi ya Uingereza kufanya mashambulizi ya angani dhidi ya Islamic State nchini Syria.

Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na uongozi wa TRA na TPA alipofanya ziara ya kustukiza Bandarini leo asubuhi.



Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na uongozi wa TRA na TPA alipofanya ziara ya kustukiza Bandarini leo asubuhi.
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa leo ameamuru kukamatwa kwa maafisa kadhaa  wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na wengine kufukuzwa kazi  baada ya kufanya ziara ya kushtukiza Bandarini na kukuta madudu ambayo hakuyafurahia.
Maafisa hao, ambao kwa sasa tunahifadhi majina ili Jeshi la Polisi liweze kuwashughulikia, wametakiwa pia kusalimisha hati zao za usafiri.
Hii imekuja baada ya kugundulika kwamba kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.







               Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa TRA na TPA

Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa 
akiagana na viongozi wa TRA na TPA.

BAT 'iliwahonga' viongozi Afrika Mashariki

Uchunguzi wa shirika la habari la BBC umegundua kuwa kampuni ya kutengeneza sigara ya British American Tobacco (BAT) imekuwa ikitoa hongo kwa wakuu serikalini katika mataifa ya kanda ya Afrika Mashariki kwa nia ya kuwashawishi kubadilisha sheria ilikulinda biashara ya tumbaku licha ya madhara yake kwa afya ya wavutaji.
Ufichuzi huo umeibuka baada ya mfanyikazi mmoja kuipatia BBC stakabadhi zinazofichua ufisadi huo.
BAT ilipoulizwa kuhusu ukweli wa madai hayo ya ufisadi iliiambia BBC kuwa
''Ukweli ni kuwa hatushiriki ufisadi kwa namna yeyote katika mataifa yeyote tunayohudumu''
Paul Hopkins, ambaye aliifanyia kazi kampuni hiyo ya BAT, nchini Kenya kwa miaka 13 anasema kuwa alianza kutoa hongo baada ya kuambiwa kuwa hiyo ni gharama ya kufanya biashara barani Afrika
"ukweli ni kwamba ikiwabidi kuvunja sheria ilikufaulu katika biashara huwa wanavunja sheria''
barua pepe zilizotumwa na Hopkins zinaonesha vipi mawasiliano yalianza na jinsi malipo yalivyotolewa.
Aidha Hopkins anaonesha jinsi BAT ilivyowapa hongo maafisa wa shirika la afya duniani WHO ambao wanasimamia udhibiti wa matumizi ya tumbaku ilikupunguza idadi ya watu wanaopoteza maisha yao kutokana na maradhi yanayotokana na matumizi ya mmea huo.
BURUNDI
Afisa mmoja wa FCTC nchini Burundi, Godefroid Kamwenubusa,na mwakilishi wa visiwa vya Comoros , Chaibou Bedja Abdou, walilipwa kiinua mgongo cha dola $3,000 (£2,000).
Wakati huohuo mwakilishi wa Rwanda, Bonaventure Nzeyimana, akatia kibindoni dola elfu $20,000.




Wote hao wamekanusha kupokea hongo kutoka kwa BAT.
RWANDA
Dakta Vera Da Costa e Silva, wa WHO, ameilaumu BAT na kusema kuwa "ni jambo la kufedhehesha sana''.
"hii ni unyama, kutumia fedha ilikupata faida huku maisha ya watu yakiangamia'' BAT sharti iadhibiwe vikali na serikali alisema bibi huyo.
BAT kimsingi iliwatumia watu waliopokea hongo kubadilisha sheria za nchi husika ilikuzuia biashara hiyo ya tumbaku isiathirike.
Kwa mfano wakala wa kampuni hiyo anasema katika moja ya nyaraka za siri kuwa Bwana Kamwenubusa atafuatilia na kufanikisha mabadiliko muhimu kabla rais wa nchi hiyo kutia sahihi na kuifanya kuwa sheria.
Comoros
Nchini Uingereza ni hatia kutoa hongo hata kama matukio hayo ya rushwa yalifanywa katika mataifa mengine.
BAT kwa upande wake inajitetea kwa kusema kuwa wafanyikazi wake walifanya makosa kinyume na maadili ya kampuni hiyo.
"Tunawahakikishia kuwa tunachunguza madai haya kwa nia ya kuadhibu wale watakaopatikana na hatia ya kukiuka maadili ya BAT''
''Wale wanaotoa madai hayo ni wafanyikazi wetu waliotimuliwa na hivyo tunahisi hizi ni njama za kulipiza kisasi''
Bwana Hopkins anasikika katika ukanda ulionaswa kisiri akimshauri wakili wa kampuni hiyo kuwa watu kadhaa watahitajika kulipwa ilikufunga vivywa vyao.
Wakili huyo Naushad Ramoly, anasikika akiuliza iwapo kuna watu wengine wanaostahili kulipwa ?''
Ramoly ambaye sasa hafanyikazi na BAT anasema kuwa hakushiriki ukiukaji wa maadili yeyote na wala hakuhusika katika shughuli zozote zinazokiuka sheria na kanuni''




Aliyeua na kuchapisha kwa Facebook kufungwa

wanaume mmoja aliyeua mkewe na kuchapisha picha yake kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook amepatikana na hatia ya mauaji.
Derek Medina mwenyeji wa Florida Marekani alipatikana na hatia ya kumpiga risasi 8 Jennifer Alfonso nyumbani kwao baada ya majibizano makali.
Kiongozi wa mashtaka wa jimbo la Miami-Dade,Katherine Rundle amesema inaudhi kuwa mwanamme mkatili anaweza kumpiga risasi mwanamke na kisha kuchapisha picha kwenye mtandao wa kijamii.


Medina alidai kuwa mkewe mwenye umri wa miaka 27 alikuwa ametishia kumdunga kisu. 

 wanaume mmoja aliyeua mkewe na kuchapisha picha yake kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook amepatikana na hatia ya mauaji.
Derek Medina mwenyeji wa Florida Marekani alipatikana na hatia ya kumpiga risasi 8 Jennifer Alfonso nyumbani kwao baada ya majibizano makali.
Kiongozi wa mashtaka wa jimbo la Miami-Dade,Katherine Rundle amesema inaudhi kuwa mwanamme mkatili anaweza kumpiga risasi mwanamke na kisha kuchapisha picha kwenye mtandao wa kijamii.









Idadi ya vijana wanaokataa kwenda shule kwa sababu ya kujishughulisha na uchumaji upakiaji wa matawi yake

Idadi ya vijana wanaokataa kwenda shule kwa sababu ya kujishughulisha na uchumaji upakiaji wa matawi yake.

Hata hivyo utafiti katika maeneo yanayokuzwa mumea huu umetambua kuwa idadi ya vijana wanaokataa kwenda shule kwa sababu ya kujishughulisha na uchumaji wa Miraa na upakiaji wa matawi yake.
''kutokana na utashi wa bidhaa hiyo,malipo ya wafanyikazi wanaoishughulikia ni ya juu mno kwa hivyo inawavutia vijana kuacha masomo alisema daktari huyo.
Daktari Lukoye Atwoli alisema kuwa miraa husababisha walaji wake kuwa na mori na hata wakati mwengine msongo wa mawazo.
Utafiti huu unafwatia ule uliofanywa mwaka uliopita na wataalamu kutoka chuo kikuu cha Nairobi kwa ushirikiano na chuo kikuu cha Konstanz cha Germany na kile cha Minnesota, Marekani uliobaini kuwa ulaji wa miraa unaathiri ubongo wa walaji wake na kusababisha msongo wa mawazo,mafadhaiko na mahangaiko ya kiakili mbali na matatizo mengine chungu nzima.

 

Utafiti:Ulaji wa miraa unapunguza nguvu za kiume

Ulaji wa Miraa unaathiri nguvu za kiume.
Utafiti uliofanywa kwa niaba ya serikali ya Kenya na wahadhiri wa chuo kikuu cha Moi kilichoko katika Bonde la ufa umebaini kuwa Majani ya miraa inayofahamika pia kama 'Mairungi' unazuia ukuaji wa manii.
Aidha ulaji wa kipindi kirefu wa miraa unafanya mbegu za kiume za wanaume kufa haraka pindi zinapowekwa kwenye uke.
Mtafiti mkuu wa chuo kikuu cha Moi, Ochiba Lukanda, anasema kuwa utafiti sawa na huo uliofanywa huko ghuba ulibaini matokeo kama hayo.
Lukanda anasema kuwa wanaume ambao wamekuwa wakila Miraa kwa kipindi kirefu na wakaacha huwa wanapata uwezo wao wa kutunga mimba.
Ulaji wa Miraa pia huwa unasababisha mshtuko wa moyo.
''Mtu anapokula mmea huu baada ya muda damu yake huaanza kwenda kwa kasi, mbali na shinikizo la damu mumea huu hausababishi saratani kama inavyodaiwa '' Dakta Lukanda